Saturday, August 23, 2014

KWELI HAKUNA JIPYA HAPA DUNIANI.....EBU TAZAMA HII ENZI YA MWALIMU!!!

Siku hizi hizi social media ndio zinakuza mambo...hawa kina LULU , WEMA walikuwepo toka kitamboooo!!!

New AUDIO | Oscar nyerere Na Dr Mfyuzi Ft Ally Nipishe - Amani | Download

Wimbo huu Umeimbwa na baadhi ya waigizaji sauti nchini yani Oscar Petro maarufu kama Oscar nyerere na Shaphii Omary maarufu kama dr.mfyuzi unaosisitiza Amani ya nchi yetu Tanzania kwa kutumia sauti ya hayati Baba wa Taifa na sauti ya raisi wa awamu ya nne dr Kikwete. Wimbo una mahadhi ya kuhutubia lakini pia una chorus iliyoimbwa na Ally Nipishe toka THT. Video ipo njiani inayotarajiwa kutoka mwishoni mwa mwezi huu wa nane 2014.BONYEZA APO CHINI KUDOWNLOAD

>>›> BONYA HAPA KUDOWNLOAD <<<<<<‹<‹

HATIMAYE DIAMOND PLATINUMZ AMETANGAZA NDOA NA MCHUMBA WAKE WA MUDA MREFU WEMA SEPETU!!!!

KUPITIA Gazeti la Mwanaspoti ambalo kwa mujibu wa takwimu za mauzo nchini ni wazi kwamba halina mpinzani, msanii wa muziki wa kizazi kipya Diamond Platinumz ametangaza ndoa na mchumba wake wa muda mrefu Wema Sepetu anayosema itafungwa hivi karibuni. Msanii huyo ghali zaidi nchini kwa sasa, ametamka hayo alipozungumza na Mwanaspoti nyumbani kwake Sinza jijini Dar es Salaam juzi Jumatano. Alisema kuna mambo mengi yaliyomchelewesha kufikia hatua hiyo, ikiwamo maandalizi kwani amepanga mashabiki wake wahudhurie harusi hiyo. “Ndoa ni kitu cha heri na baraka, lakini kitu kinachofanya kidogo mambo yachelewe ni kwamba sisi au mimi ni mtu ninayefahamika, kwa hiyo hata ndoa yangu watu wengi wanatamani waihudhurie,” alisema Diamond. Pia amesisitiza kwamba ndoa si jambo la masihara kwani ni tendo la kiimani na ndio maana amekuwa makini katika mipango yake. “Nataka kila kitu kishuhudiwe na mashabiki, ninaweza hata kuifanyia Uwanja wa Taifa,” aliongeza. “Unajua nilishindwa kufanya mambo haya haraka kwa sababu wengi nadhani wangeamini kwamba ninafanya hivyo ili kutafuta umaarufu zaidi, tunataka tufanye kiusahihi yasije tokea mambo kama ya Instagram tunataka tuje kuwa mfano wa kuigwa.” Alipoulizwa tarehe ya ndoa hiyo Diamond alisema: “Nilishasema ni hivi karibuni, unajua siku zote vitu vya kheri waswahili wanasema lazima uvifiche, hata Mwenyezi Mungu naye anasema anampenda mtu aliye na siri, lazima vitu vingine uvifiche ili vipate kufanikiwa. Wakati mwingine kunakuwa na husda, hasidi kwa hiyo ukiviweka wazi sana vinaweza kutofanikiwa.” Taarifa kwamba Diamond hataoa zilisambaa na kudaiwa kumchefua mchumba wake Wema Sepetu ambapo katika mahojiano mkali huyo wa wimbo ‘Mdogo Mdogo’ alisema: “Kwanza sikuwahi kusema siwezi kuoa, nilishtushwa na gazeti hilo, nilisikitika kwa kweli na iliniuma sana, lakini nikaona nikijibu nitaonekana kwamba sina adabu, kwa sababu siku zote anayeanza huwa haonekani lakini anayemaliza. Pia siwezi kubishana na vyombo vya habari, mwisho wa siku ni watu haohao nitawategemea wanifanyie kazi zangu,” alisema. Hata hivyo Diamond alisema mchumba wake anaumizwa na vichwa vya habari ambavyo vimekuwa mwiba kwake. “Hata hivyo magazeti yetu tumeshayazoea jinsi yanavyoandika, wakati mwingine inakuwa kama chachandu au kufurahisha baraza,” aliongeza. Kuhusu taarifa kwamba ameachana na mchumba wake huyo, alisema: “Hatuna tatizo watu wengi wanasema tumeachana, lakini hatujaachana na hatuwezi kujibishana. “Sijui nikujibu nini kwa sababu kila nitakachokujibu utaona namsifia kwa sababu yule ni mchumba wangu.

HUYU NDIO KIONGOZI WA FREEMASON AFRIKA MASHARIKI, NI MTANZANIA. AFUNGUKA MENGI...HADI SWALA LA KANUMBA. INGIA HAPA

Ukisoma aliyofunguka utaogopa. Azungumzia hadi Msanii kanaumba aliyvyoingia.

Story nzima  >>>>>>ingia apa <<<<<<<<<<<<<<<<<

CHEKI CHELSEA WANAVYOJIFUA KUIWINDA LEICESTER CITY LEO

KATIKA MECHI YA KWANZA YA LIGI KUU ENGLAND, CHELSEA ILIANZA KWA KUITWANGA BURNLEY 3-1; SASA INAJIWINDA DHIDI YA LEICESTER LEO JUMAMOSI NA KWA KOCHA JOSE MOURINHO ATAKUWA ANAKUTANA NAYO KWA MARA YA KWANZA

RASMI, BALOTELLI ATUA LIVERPOOL, MASHABIKI WAJAZANA KUMSHUHUDIA

MSHAMBULIAJI WA ZAMANI WA MAN CITY ALIYEKUWA AKIKIPIGA AC MILAN, MARIO BALOTELLI AMEFUZU VIPIMO NA SASA UNAWEZA KUSEMA NI MCHEZAJI WA LIVERPOOL. MASHABIKI WAMEJITOKEZA KWA WINGI KUMLAKI INGAWA HATACHEZA MECHI DHIDI YA MAN CITY, JUMATATU USIKU. MSHAHARA WAKE KWA WIKI UTAKUWA NI PAUNI 125,000.

ULEVI MBAYA, ANGALIA UNAVYOMMALIZA SHUJAA WA ENGLAND, SURA IMEKUWA KA' KINYAGO

GAZZA (KULIA) WAKATI AKIWA FITI ANAITUMIKIA ENGLAND.
AKICHUKULIWA NA POLISI BAADA YA KUKUTWA AMELALA NJE YA NYUMBANI KWAKE KUTOKANA NA KUZIDIWA NA KILEVI. MARA KADHAA AMEKUWA AKITIBIWA LAKINI GAZZA AMESHINDWA KUJIONDOA KWENYE ULEVI KUPINDUKIA. ALIKUWA NYOTA WA TIMU YA TAIFA YA ENGLAND, LAKINI ULEVI KUPINDUKIA UNAMTAFUNA

ANGALIA TANZANIA ELEVEN WANAVYOPIGA BATA NDANI YA SAPPHIRE COURT KABLA YA KUIVAA MADRID LEO

NSAJIGWA, NYENGE NA MASATU.
KIKOSI CHA TANZANIA ELEVEN WAKIJIACHIA KWA MISOSI YA NGUVU KWA MGAHAWA WA HOTELI YA SAPPHIRE COURT YA JIJINI DAR ES SALAAM AMBAKO WAMEWEKA KAMBI KUJIWINDA DHIDI YA WAKONGWE WA REAL MADRID AMBAO WATAWAVAA LEO KWENYE UWANJA WA TAIFA JIJINI DAR KATIKA MECHI YA KIRAFIKI INAYOSUBIRIWA KWA HAMU KUBWA NA MASHABIKI
LUNYAMILA NA ATHUMANI CHINA.
IDDI MOSHI MNYAMWEZI NA MAXIME.
CHINA

Credit salley ally

Haya ndo matokeo ya mechi kati ya ATLETICO MADRID VS REALMADRID, super cup

Wakati wakongwe wao wakitarajiwa kucheza mechi ya kirafiki leo jijini Dar es Salaam, Real Madrid imeshindwa kuonyesha kuwa wanaweza baada ya kuchapwa bao 1-0 na wapinzani wao wakubwa Atletico Madrid. Kipigo hicho cha bao 1-0 katika mechi ya pili ya Super Cup, maana yake Atletico wameibuka mabingwa kwa jumla ya mabao 2-1 baada ya sare ya 1-1 katika mechi ya kwanza ndani ya Camp Nou. Muuaji wa jana alikuwa na Mario Mandzukic ambaye amejiunga na Atletico akitokea Bayern Munich ambaye alifunga bao hilo katika dakika ya 2 tu. Pamoja na juhudi za Kocha Carlo Ancelotti kumuingiza Cristiano Ronaldo katika kipindi cha pili, bado Madrid haikuweza kupindua matokeo. Kiungo Luca Modric alilambwa kadi mbili za njano na kuwa nyekundu. NA MDADISIBLOG/FESTOSAIMON

MSAFARA WA MWISHO WA REAL MADRID ULIVYOTUA DAR, LEO TAIFA PATAPENDEZA

Magwiji wa Real wakisubiri usafiri kuelekea Bahari Beach
Watu walijitokeza kuwapokea
Wanaelekea kwenye basi la Azam FC kwa safari ya hotelini
Msafara wa mwisho wa Real Madrid baada ya kuwasili Dar es Salaam jana jioni tayari kwa mchezo wa leo dhidi ya magwiji wa Tanzania Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.