Friday, August 15, 2014

DIAMOND AHANDIKA UJUMBE MZITO UNAOMLENGA MTU FULANI HAPA BONGO

Story ya ni kuhusu ujumbe mrefu aliondika Diamond kupitia ukurasa wake wa instagram. Ujumbe huo unaonekana unaenda kwa msanii fulani japokuwa hakuweka wazi ni msanii gani.

Diamond aliweka post hii na baada ya muda mfupi aliifuta lakini maneno yote yalikuwa yanasomeka hivi.

“Nafkiri ningewaona kweli Mnaakili na Mapenzi ya dhati kwa Msanii wenu… kama mngemshauri apunguze Mashoga wapenda anasa na apunguze Stareh zisizo na Faida, wenda ingemsaidia Pesa kuzitumia kwenye kufanya kazi na kuleta maendeleo badala ya kuwapa viwanda vya pombe…

Mimi kama bwana, wajibu wangu ni kuhakikisha Mpenzi wangu anakula vizuri, anavaa vizuri, analala vizuri, na kumuwezesha mtaji wa kufanyia kazi…. Waswahili wanasema Mchungaji bora anatakiwa kuhakikisha anampeleka Ng’ombe wake Kwenye Maji safi….ila yeye ng’ombe mwenyewe ndio anatakiwa aamue kunywa maji!!!!! Au mnataka nikishampa mtaji niache kufanya na show tena na kuigiza nimuigizie mie ???? Nisiende Studio nikae dukani nimuuzie mie????.. ni juhudi zako kwanza!… leo hii mimi Hata ningepewa Mamilioni ya mamilioni kama nisingekuwa na moyo wa mie mwenyewe kwanza kutaka kujituma na kupenda kufanya kazi yangu nisingefikia hapa nilipo! ….Mxieeeeeeeew!�� Kama nimekuchefua Lamba ndimu Usitapike”.

 ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG HII ILA TUNAOMBA UJIUNGE NASI KWA KUBONYA HAPA 


Posted via Blogaway

YANGA SC WAKIJUA HII, WATAMLAANI KWELI KWELI MUSONYE

Katibu wa CECAFA, Nicholas Musonye kushoto ambaye aliiondoa klabu ya Yanga SC kwenye michuano ya Kombe la Kagame kwa kutaka kuleta timu ya vijana, akizungumza na Ofisa wa Sekretarieti ya bodi hiyo, Veronica Lusiichi kulia Uwanja wa Nyamirambo, Kigali, Rwanda jioni ya leo wakati mechi za michuano hiyo zikiendelea. Azam FC ilipewa nafasi ya Yanga SC.
Ofisa mwingine wa Mamelodi, Mandla Mazibuko akifuatilia vipaji Uwanja wa Nyamirambo. Kulia ni Mtangazaji kutoka Tanzania, Ibrahim Masoud 'Maestro'
Ofisa wa Idara ya kusaka vipaji ya klabu ya Mamelodi Sundowns ya Afrika Kusini, Russel Molefe kulia akizungumza na Mwandishi wa Habari, Somoe Ng'itu kutoka Tanzania. Yanga SC ingebahatisha kuuza nyota wake klabu hiyo kama wangewavutia wasaka vipaji hawa.

 ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG HII ILA TUNAOMBA UJIUNGE NASI KWA KUBONYA HAPA 


Posted via Blogaway

Thursday, August 14, 2014

MAHAKAMA YA SOKA YAMPUNGUZIA ADHABU LUIS SUAREZ

Mahakama ya Soka ya Kimataifa CAS, imekubali kupunguza adhabu ya kumfungia miezi minne Luis Suarez wa Barcelona baada ya kumuuma Giorgio Chiellini wa Italia wakati wa Kombe la Dunia.

CAS imetoa nafuu kwa Suarez na sasa Barcelona rasmi itamtambulisha Jumatatu na atapewa ruksa ya kufanya mazoezi na wenzake.

Mambo ambayo yamepunguzwa na yale yanayobaki kuwa adhabu ni kama yafuatayo.

Suarez ruhusa:
- Kufanya mazoezi na Barcelona.
- Kutambulishwa na Barcelona.
- Kucheza mechi za kirafiki, si zile za mashindano.
- Kucheza mechi za kirafiki za Uruguay dhidi ya Japan, Korea na Saudi Arabia katika miezi ya Septemba na Oktoba
- Kuhudhuria mechi uwanjani.
- Kuhudhuria shughuli za matangazo zinazoihusisha Barcelona.

Suarez si ruhusa:

- Kucheza mechi yoyote ya mashindano akiwa na Barca hadi Oktoba 26.
- Kuichezea Uruguay mechi yoyote hadi zifikie mechi nane.

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NA BLOG HII ILI KILA TUKIPATA HABARI ZIKUFIKIE KIRAHISI 

By mdadisiblog/festosaimon


Posted via Blogaway

TIMU YA YANGA YA ENDELEZA KUIMARISHA SAFU YA ULINZI KWA KUIPIGA BAO SIMBA KATIKA USAJILI

Na Prince Akbar, DAR ES SALAAM YANGA SC imefanikiwa kumpata beki chipukizi wa JKT Ruvu, Edward Charles baada ya kukamilisha taratibu zote za usajili wake kutoka timu hiyo ya Jeshi la Kujenga Taifa na kumsainisha Mkataba wa miaka mitatu.

Yanga SC kwa miezi miwili sasa imekuwa ikisotea saini ya mchezaji huyo kwa kuanzia kufuata taratibu za kuvunja mkataba wake jeshini- hadi leo ilipokamilisha.

Viongozi wa Yanga SC wakiongozwa na Francis Kifukwe leo walikuwa na kikao cha mwisho na uongozi wa JKT juu ya suala la uhamisho wa mchezaji huyo na mambo yamekwenda vizuri.

Beki huyo alikuwa pia anawaniwa na mahasimu Simba SC, ambao jitihada zao ziligonga ukuta mapema, baada ya kuambiwa wapinzani wao Yanga SC, wamepiga hatua kubwa katika kufukuzuia huduma za chipukizi huyo.

Edward sasa atajiunga na Yanga SC mara moja chini ya kocha Mbrazil, Marcio Maximo kuanza maandalizi ya msimu mpya.

Ni Maximo aliyewasukuma viongozi wa Yanga SC kufukuzia haraka saini ya mchezaji huyo baada ya kutovutiwa na uchezaji wa beki wa sasa wa kushoto wa klabu hiyo, Oscar Joshua. Edward Charles ni kati ya chipukizi waliopo timu ya taifa ya wakubwa kwa sasa, Taifa Stars chini ya kocha Mholanzi, Mart Nooij ambao wanainukia vizuri.

Ni mkabaji mzuri, ana nguvu, kasi- mbinu za anapokuwa na mpira na asipokuwa nao na pia hupanda vizuri kushambulia na kurudi kwa haraka. Anasifika kwa kupiga krosi nzuri pamoja na mpira iliyokufa.

 BONYEZA HAPA ILI UJIUNGE NA BLOG HII HUPATE HABARI KIRAHISI 

BREAKING NEWS: PHIRI ASAINI MKATABA WA MWAKA MMOJA KUINOA SIMBA

Kocha wa Simba, Patrick Phiri amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuifundisha Simba.

Phiri raia wa Zambia amesaini mkataba huo leo kwenyeHoteli ya Regency. Phiri ameiambia mdadisiblog, mkataba huo unampa ruhusa kuitumikia Simba kwa matumaini makubwa. “heshima ya Simba kwangu ni kubwa sana, ingawa nilikuwa nina mipango mingine, lakini nimekubali kurejea.

“Kazi haitakuwa lahisi, lakini vizuri kwamba sasa tumeingia mkataba mpya wa kazi, ninaamini mambo yatakwenda vizuri,” alisema Phiri.

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NASI 

SPURS YASAJILI BEKI LA KULIA LA MAREKANI MIAKA MINNE

KLABU ya Tottenham imekamilisha usajili wa mwanasoka wa kimataifa wa Marekani, DeAndre Yedlin kwa Mkataba wa miaka minne. Beki huyo wa kulia mwenye umri wa miaka 21, atabaki Seattle Sounders kabla ya kujiunga na kikosi cha Mauricio Pochettino msimu wa 2015/2016. Akizungumza na tovuto ya klabu hiyo, Yedlin alisema; "Nimefurahishwa sana kuja Ligi Kuu ya England na kujishindanisha dhidi ya baadhi ya wachezaji bora duniani,".

 BONYEZA HAPA KUJIUNGA NA BLOG HII 

WAKATI PHIRI AMETUA DAR, ANGALIA LOGA ALIVYOIAGA DAR ES SALAAM

Wakati Kocha mpya wa Simba, Patrick Phiri raia wa Zambia ametua nchini, angalia aliyekuwa kocha wa timu hiyo, Zdravko Logarusic alivyoliaga jiji la Dar. Kupitia mtandao wa Facebook,

Loga ametupia picha mbili huku akiandika “by by Tanzania), akimaanisha bye bye Tanzania. Loga ameiaga Tanzania kwa picha hizo, moja akiwa ndani Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere (JNIA) akiwa amepiga shati lake la pink na mkononi ameshikilia kinywaji aina ya Redbull.

Picha ya pili, Loga anaonekana kiwa amekaa kwenye beki, hapo ni kabla ya kuingia ndani ya uwanja huo.

Kocha huyo ameondoka na dege la Shirika la Ndege la Tukish. Kama safari yake imekwenda vizuri, tayari Loga atakuwa amewasili kwao salama.

 ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG HII ILA TUNAOMBA UBONYE HAPA KUJIUNGA NASI 

Mdadisi blog/festo saimon

Vincent kompany ajitia kitanzi kizito Man city

NAHODHA wa Manchester City, Vincent Kompany amesaini Mkataba mpya wa miaka mitano na mabingwa hao wa Ligi Kuu ya England.

Habari za Kompany kupewa Mkataba mpya ambao inaaminika utmfanya sasa awe analipwa Pauni 130,000 kwa wiki, zinakuja saa 24 baada ya kiungo David Silva pia kusaini Mkataba mpya utakaomuweka katika klabu hiyo mwaka 2019.

Beki huyo kivutio wa Ubelgiji, ameiongoza Man City kutwa ubingwa wa Ligi Kuu ya England mara mbili katika miaka mitatu iliyopita, pamoja na mataji ya FA na Capital One Cup. Na Kompany, mwenye umri wa miaka 28, anataka kushinda mataji mengine matatu kabla ya kuondoka Etihad.

 ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG HII ILA TUNAOMBA UJIUNGE NASI KWA KUBONYA HAPA 

Mdadisiblog/festo saimon

BORUSSIA DORTMUND WAIFUMUA BAYERN MUNICH 2-0 NA KUTWAA SUPER CUP YA UJERUMANI

Wababe; Wachezaji wa Borussia Dortmund wakiwa na taji lao la Super Cup ya Ujerumani, baada ya kuifunga Bayern Munich mabao 2-0 jioni ya leo, wafungaji Hendrikh Mkhitaryan na Pierre- Emerick Aubameyang.

 UNAPENDA HABARI ZA KIMICHEZO ZIKUFIKIE KIRAHISI ZAID BONYA HAPA KUJIUNGA NASI 

Hii ni ishara kwamba Vidal anaweza kutua Manchester united

KIUNGO Arturo Vidal anayetakiwa na Manchester United ameonyesha ishara fulani, baada ya kusaini jezi ya shabiki wa Mashetani hao Wekundu akiwa kwenye ziara na klabu yake, Juventus nchini Australia.

Vidal, ambaye amekuwa akihusishwa na kuhamia Old Trafford kwa muda sasa baada ya nyota huyo wa Chilea kung'ara msimu uliopita, amekuwa akishawishiwa na wachezaji wenzake kubaki Italia.

Kiungo mwingine wa Juventus, Paul Pogba alisema wiki iliyopita kwamba anatumaini Vidal atabakia katika klabu hiyo, licha ya kutakiwa na United, lakini hali inaonekana kuwa tofauti baada ya kusaini jezi ya United.

 WEWE NI MWANAMICHEZO NA UNAPENDA UPATE HABARI ZA KIMICHEZO PUNDE ZINAPOTUFIKIA BONYA HAPA 

Mdadidiblog/festo saimon