KIUNGO Arturo Vidal anayetakiwa na Manchester United ameonyesha ishara fulani, baada ya kusaini jezi ya shabiki wa Mashetani hao Wekundu akiwa kwenye ziara na klabu yake, Juventus nchini Australia.
Vidal, ambaye amekuwa akihusishwa na kuhamia Old Trafford kwa muda sasa baada ya nyota huyo wa Chilea kung'ara msimu uliopita, amekuwa akishawishiwa na wachezaji wenzake kubaki Italia.
Kiungo mwingine wa Juventus, Paul Pogba alisema wiki iliyopita kwamba anatumaini Vidal atabakia katika klabu hiyo, licha ya kutakiwa na United, lakini hali inaonekana kuwa tofauti baada ya kusaini jezi ya United.
WEWE NI MWANAMICHEZO NA UNAPENDA UPATE HABARI ZA KIMICHEZO PUNDE ZINAPOTUFIKIA BONYA HAPA
Mdadidiblog/festo saimon
0 comments:
Post a Comment