Thursday, August 14, 2014

MAHAKAMA YA SOKA YAMPUNGUZIA ADHABU LUIS SUAREZ

Mahakama ya Soka ya Kimataifa CAS, imekubali kupunguza adhabu ya kumfungia miezi minne Luis Suarez wa Barcelona baada ya kumuuma Giorgio Chiellini wa Italia wakati wa Kombe la Dunia.

CAS imetoa nafuu kwa Suarez na sasa Barcelona rasmi itamtambulisha Jumatatu na atapewa ruksa ya kufanya mazoezi na wenzake.

Mambo ambayo yamepunguzwa na yale yanayobaki kuwa adhabu ni kama yafuatayo.

Suarez ruhusa:
- Kufanya mazoezi na Barcelona.
- Kutambulishwa na Barcelona.
- Kucheza mechi za kirafiki, si zile za mashindano.
- Kucheza mechi za kirafiki za Uruguay dhidi ya Japan, Korea na Saudi Arabia katika miezi ya Septemba na Oktoba
- Kuhudhuria mechi uwanjani.
- Kuhudhuria shughuli za matangazo zinazoihusisha Barcelona.

Suarez si ruhusa:

- Kucheza mechi yoyote ya mashindano akiwa na Barca hadi Oktoba 26.
- Kuichezea Uruguay mechi yoyote hadi zifikie mechi nane.

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NA BLOG HII ILI KILA TUKIPATA HABARI ZIKUFIKIE KIRAHISI 

By mdadisiblog/festosaimon


Posted via Blogaway

0 comments:

Post a Comment