Kocha wa Simba, Patrick Phiri amesaini mkataba wa mwaka mmoja kuifundisha Simba.
Phiri raia wa Zambia amesaini mkataba huo leo kwenyeHoteli ya Regency. Phiri ameiambia mdadisiblog, mkataba huo unampa ruhusa kuitumikia Simba kwa matumaini makubwa. “heshima ya Simba kwangu ni kubwa sana, ingawa nilikuwa nina mipango mingine, lakini nimekubali kurejea.
“Kazi haitakuwa lahisi, lakini vizuri kwamba sasa tumeingia mkataba mpya wa kazi, ninaamini mambo yatakwenda vizuri,” alisema Phiri.
0 comments:
Post a Comment