Saturday, August 30, 2014
|
Imepita zaidi ya wiki moja tangu klabu ya
Manchester United ilipokamilisha usajili wa
beki wa kimataifa wa Argentina Marcos Rojo
kutoka klabu ya Sporting Lisbon – lakini cha
ajabu mchezaji huyo amekuwa haonekani
kwenye mechi za United.
Leo hii imefahamika kwamba mchezaji huyo
bado hajapata kibali cha kumuwezesha
kufanya kazi nchinin UK – kitu kinachomfanya
timu yake ishindwe kupata idhini ya premier
league kumchezesha mchezaji huyo.
Mwanzoni kulikuwa wasiwasi kwamba utata
wa kisheria uliopo kati ya klabu yake ya
zamani Sporting dhidi ya kampuni ya Doyen
Sports ambayo ilikuwa inamiliki asilimia 75 ya
haki zake za usajili.
Lakini leo hii kocha wa Man united Louis van
gaal amethibitisha mchezaji huyo amekwama
kutokana na kibali cha kazi na sasa yupo
nchini Hispania ambapo ndio kuna ubalozi wa
Argentina akifuatilia kibali hicho.
Hata hivyo Van Gaal amesema suala hilo sasa
halitachukua muda mrefu, pia akathibitisha
kwamba Angel Dimaria anaweza kuanza kesho
kwenye mchezo dhidi ya Burnley. |
Posted via Blogaway
0 comments:
Post a Comment