Saturday, August 30, 2014
|
HATIMAYE mshambuliaji Fernando Torres
amemaliza miaka yake mitatu na nusu migumu
Chelsea kwa kukubali kuhamia AC Milan.
Mchezaji huyo wa Hispania anakwenda kuziba
pengo la Mario Balotelli ambaye Milan
imemuuza kwa Pauni Milioni 16 Mtaliano huyo
Liverpool.
Wakala wa Torres alifanya mazungumzo na
Milan Alhamisi asubuhi na mshambuliaji huyo
amekubali kujiunga na vigogo hao wa Italia
kwa miaka miwili.
Amechuja: Licha ya kusajiliwa kwa Pauni
Milioni 50 kutoka Liverpool, Torres amemudu
kufunga mabao 45 tu katika mechi 172
alizocheza Chelsea
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30
anahamia San Siro kwa mkopo wa miaka
miwili.
Torres aliyetua Stamford Bridge kwa dau la
Pauni Milioni 50 alikuwa amebakiza miaka
miwili katika mkataba wake wa Pauni 150,000
kwa wiki Stamford Bridge na inaaminika
wawakilishi wake walipatana kiasi hicho hicho
cha mshahara kabla ya mchezaji huyo kukubali
uhamisho huo.
Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho
alikuwa radhi kumuacha Torres kabla ya
dirisha la usajili kufungwa Jumatatu ili kupata
nafasi ya kusajili mshambuliaji mwingine na
Loic Remy sasa yupo kwenye nafasi nzuri ya
kutua Magharibi mwa London kutoka Queens
Park Rangers. |
Posted via Blogaway
0 comments:
Post a Comment