Saturday, August 30, 2014

HATIMAYE TORRES AONDOKA CHELSEA AENDA TIMU HII

HATIMAYE mshambuliaji Fernando Torres amemaliza miaka yake mitatu na nusu migumu Chelsea kwa kukubali kuhamia AC Milan. Mchezaji huyo wa Hispania anakwenda kuziba pengo la Mario Balotelli ambaye Milan imemuuza kwa Pauni Milioni 16 Mtaliano huyo Liverpool. Wakala wa Torres alifanya mazungumzo na Milan Alhamisi asubuhi na mshambuliaji huyo amekubali kujiunga na vigogo hao wa Italia kwa miaka miwili. Amechuja: Licha ya kusajiliwa kwa Pauni Milioni 50 kutoka Liverpool, Torres amemudu kufunga mabao 45 tu katika mechi 172 alizocheza Chelsea Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 30 anahamia San Siro kwa mkopo wa miaka miwili. Torres aliyetua Stamford Bridge kwa dau la Pauni Milioni 50 alikuwa amebakiza miaka miwili katika mkataba wake wa Pauni 150,000 kwa wiki Stamford Bridge na inaaminika wawakilishi wake walipatana kiasi hicho hicho cha mshahara kabla ya mchezaji huyo kukubali uhamisho huo. Kocha wa Chelsea, Jose Mourinho alikuwa radhi kumuacha Torres kabla ya dirisha la usajili kufungwa Jumatatu ili kupata nafasi ya kusajili mshambuliaji mwingine na Loic Remy sasa yupo kwenye nafasi nzuri ya kutua Magharibi mwa London kutoka Queens Park Rangers.

Posted via Blogaway

0 comments:

Post a Comment