Wednesday, August 13, 2014

NI PATRICK PHIRI, KOCHA MPYA WA SIMBA SC

Na Baraka Mbolembole, Dar es Salaam, Alikuja akaondoka bila kuaga, alirudi akaondolewa kwa sababu, sasa anarejea tena kwa mara ya tatu klabuni Simba SC kama mkufunzi mkuu wa idara ya ufundi.

Namzungumzia, kocha raia wa Zambia, Patrick Phiri ambaye anatua nchi leo akitokea kwao kujiunga na Simba kwa mara ya tatu katika kipindi cha miaka kumi’. Phiri ameandaliwa mkataba wa miaka miwili na atasaini mara baada ya kuafikiana kuhusu mambo binafsi.

Ni kocha mzuri ambaye wachezaji wengi hupenda kufanya naye kazi. Mahitaji ya lazima ya timu ni kupata ushindi kadri inavyotakiwa lakini hilo litawezekana kama mahusiano ya kijamaa yataboreshwa kati ya uongozi na kocha, kwa maana ya kumuachia majukumu yote ya ufundi mwalimu.

Mara ya kwanza, Phiri aliondoka na hakutaka kurejea kuifundisha timu hiyo alipotwaa ubingwa wa Tanzania Bara mwaka, 2004 na ilikuja kugundulika kuwa mwalimu huyo alichukizwa na kitendo cha baadhi ya viongozi kumuingilia katika majukumu yake ya upangaji wa timu na kumchagulia wachezaji wa kuwatumia.

Tabia hiyo bado ipo na inaendelea kuwahukumu makocha wengi klabuni Simba na hata, Mcroatia, Zdravko Logarusic ameondoka kwa sababu hizo.

Heshima ya mtu inategemea jitihada zake za ufanyaji wa kazi na kutimiza majukumu yake. Kupendana, kuheshimiana kindugu, viongozi wanatakiwa kuwaamini walimu ambao wamekuwa wakipewa kazi na kuwaacha wafanye kazi yao.

Simba wanatakiwa kuishi maisha ya kijamaa ambayo kila mtu, mchezaji, kiongozi na benchi la ufundi anatakiwa kujua wajibu wake wa uwepo klabuni. Anaijua Simba, amewahi kufanya kazi, na ana mafanikio makubwa, ni sababu tatu ambazo, Zacharia Hans Poppe amesema zimewashawishi kumrejesha kocha huyo bora wa Zambia, mwaka, 1999.

Ni ukweli ulio wazi kuwa rekodi ya Phiri ndani ya uwanja ni bora pengine kuliko walimu wote ambao wamewahi kufanya kazi klabuni hapo. Phiri alichukua nafasi ya Mkenya, James Siang’a mwaka, 2004 na aliweza kuifanya timu hiyo kuwa imara katika mashambulizi huku akiwatumia wachezaji wa nafasi ya kiungo katika safu ya mashambulizi. Shaaban Kisiga, Athumani Machuppa, Nico Nyagawa, Mussa Hassan Mgosi nyota hao walikuwa wachezaji wa kutegemewa katika ufungaji.

Phiri ambaye amewahi kucheza michuano ya AFCON, 1978 na 1982 pia amewahi kushiriki michuano hiyo kama kocha mkuu wa Zambia, mwaka, 2008 nchini Ghana ni mtu asiyeishiwa sababu za kwenda nyumbani mara kwa mara hali ambayo imekuwa ikiathiri utendaji wa timu ndani ya uwanja.

Mara ya mwisho alipoondoka klabuni, Simba alichukizwa na kitendo cha kuingiliwa katika majukumu yake na hivyo kuamua kutoongeza mkataba baada ya kufanya kazi kwa miaka miwili mfululizo na kuwa kocha aliyekaa kwa muda mwingi klabuni hapo katika kipindi cha miaka kumi iliyopita.

Trott Moloto alidumu kwa mwezi mmoja baada ya kuchukua nafasi ya Phiri mapema, 2005.

 UNAPENDA MICHEZO BHAAS BONYA APA UJIUNGE NASI 

RONALDO APIGA ZOTE MBILI REAL MADRID IKIUA 2-0 NA KUTWAA NDOO KUBWA KULIKO ZOTE ZA UEFA

Wafalme wa Ulaya; Wachezaji wa Real Madrid wakifurahia na taji lao la Super Cup ya UEFA leo
Magalactico wapya: Kikosi kipya cha kwanza cha Real Madrid kilichotwaa Super Cup leo
Mambo safi kabisa: Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kuifungia Real Madrid Uwanja wa Cardiff City

MABAO mawili ya Cristiano Ronaldo, moja kila kipindi yametosha kuipa Real Madrid ushindi wa 2-0 dhidi ya Sevilla, zote za Hispania Uwanja wa Cardiff City mjini Cardiff na kutwaa Super Cup ya UEFA. Sifa zimuendee nyota wa Wales, Gareth Bale aling'ara akicheza kwenye ardhi ya nyumbani na kutoa mchango mkubwa katika ushimdi huo.

Ronaldo alifunga bao la kwanza dakika ya 30 na la pili dakika ya 49. Kikosi cha Real Madrid kilikuwa: Casillas, Carvajal, Pepe, Sergio Ramos, Fabio Coentrao, Kroos, Rodriguez, Modric, Bale, Benzema, Ronaldo. Sevilla: Beto, Coke, Pareja, Fazio, Fernando Navarro, Alex Vidal, Krychowiak, Carrico, Vitolo, Suarez, Bacca.

 KAMA WEWE UNAPENDA USIPITWE NA HABARI MBALIMBALI ZA KIMICHEZO BONYA HAPA 

Credit binzubery

VAN GAAL AENDELEZA MARAHA MAN UNITED, YAICHAPA 2-1 VALENCIA

Marouane Fellaini akiifungia Manchester United bao la ushindi dhidi ya Valencia
Shujaa wa leo: Fellaini (wa tatu kulia) akipongezwa na wenzake baada ya kuifungia Manchester United bao la ushindi

KOCHA Louis van Gaal ameendelea kuwapa raja mashabiki wa Old Trafford baada ya Manchester United leo kuifunga Valencia mabao 2-1 katika mchezo wa kirafiki.

Sifa zimuendee Marouane Fellaini aliyefunga bao la ushindi dakika ya 90 na ushei katika mchezo ambao, Wayne Rooney alikosa penalti kipindi cha kwanza iliyookolewa na Diego Alves.

United ilitangulia kupata bao kupitia kwa Darren Fletcher dakika ya 49 kabla ya Rodrigo kuisawazishia Valencia dakika ya 71. Kikosi cha Manchester United: De Gea; Jones, Smalling, Blackett; Young, Fletcher, Herrera, James; Mata; Rooney, Hernandez Valencia: Alves; Barragan, Vezo, Otamendi, Gaya; Parejo, J. Fuego, Andre Gomes; Feghouli, Alcacer, Rodrigo

 KAMA WEWE N MWANAMICHEZO NA UNAPENDA USIPITWE NA HABARI MBALIMBALI BONYA HAPA 

DIEGO COSTA AANZA MAMBO CHELSEA...APIGA ZOTE MBILI THE BLUES IKIICHAPA REAL 2-0

Onyo mapema: Diego Costa akisherehekea baada ya kuifungia Chelsea bao la kwanza Uwanja wa Stamford Bridge

MABAO ya mawili ya mapema kipindi cha kwanza ya Diego Costa yameipa Chelsea ushindi wa 2-0 dhidi ya Real Sociedad ya Hispania katika mchezo wa kirafiki kujiandaa na msimu.

Akicheza kwa mara ya kwanza kwenye Uwanja wa Stamford Bridge tangu aiongoze timu yake ya zamani, Atletico Madrid kuifunga timu ya Jose Mourinho katika Nusu Fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Costa alihitaji dakika nane tu kuiteketeza Real Sociedad.

Alifunga dakika ya kwanza na saba na sasa anafikisha jumla ya mabao manne aliyoifungia Chelsea tangu ajiunge nato akitokea Atletico mwezi uliopita.

Kikosi cha Chelsea kilikuwa; Courtois, Ivanovic/Zouma dk82, Cahill/Azpilicueta dk45, Terry/Christiansen dk86, Ake/Luis dk45,Ramires/Oscar dk45, Matic/Van Ginkel dk82, Fabregas/Mikel dk71, Schurrle/Willian dk45, Costa/Torres dk60 na Hazard/Salah dk82. Real Sociedad: Zubikarai, Zaldua/C. Martínez dk59, Ansotegi/Mikel dk11, Inigo Martinez, De la Bella/Yuri dk72, Markel/Elustondo dk59, R.Pardo/A.Oyarzun dk72, Granero/Chory dk65, X.Prieto/Hervías dk72, Canales/ Hernandez dk72 na Agirretxe/Estrada dk65

 KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BONYEZA HAPA ILI KILA TUKIPATA HABARI ZA KIMICHEZO ZIKUFIKIE KIRAHISI 

Picha: Kampuni ya Japan yatengeneza ‘midoli ya mapenzi’ yenye muonekano halisi wa mwanamke anayevutia!

Kampuni moja ya nchini Japan imedai kufanikiwa kutengeneza midoli ya ngono ‘sex dolls’ yenye muonekano halisi wa mwanamke ambayo huwa na ngozi ya mwili kama ya binadamu na macho kama ya ukweli.

Mdoli wa ngono Orient Industry imesema ni ngumu kuitofautisha midoli hiyo na msichana halisi pale unapoitazama kwa mara ya kwanza.

Midoli hiyo imepewa jina la ‘Dutch Wives’, na matangazo ya midoli hiyo yanasema kuwa iwapo mwanaume akifanya nayo mapenzi hawezi kumtamani mwanamke halisi tena.

Bei ya midoli hiyo ni £1,000 ( zaidi ya shilingi milioni 2.7) kwa kila mmoja. Midoli hiyo imetengenezwa kwa kuweka viungo ambavyo vinamfanya mtumiaji kuigeuza katika position atakayo.
KAMA BADO UJAJIUNGA NASI           BONYEZA HAPA 

KAVUMBANGU AINUSURU AZAM KULALA KWA WASUDAN

Mkombozi; Didier Kavumbangu ameifungia bao la kusawazisha Azam FC leo Kigali

Na Mahmoud Zubeiry, KIGALI AZAM FC imepunguzwa kasi katika Kombe la Kagame, baada ya kulazimishwa sare ya mabao 2-2 na Atlabara ya Sudan Kusini jioni hii Uwanja wa Stade de Kigali, Nyamirambo mjini hapa.

Mshambuliaji wa zamani wa Yanga SC, Didier Kavumbangu aliinusuru Azam kuzama katika mchezo huo wa Kundi A Klabu Bingwa Afrika Mashariki na Kati, baada ya kuifungia bao la kusawazisha dakika ya 86, baada ya krosi ya Shomary Kapombe.

Azam ilikwenda kupumzika ikiwa inaongoza kwa bao 1-0 lililofungwa na kiungo Kipre Michael Balou kwa shuti la mpira wa adhabu kutoka umbali wa mita 20, baada ya pacha wake, Kipre Herman Tchetche kuangushwa.

Atlabara ilirudi vizuri kipindi cha pili na kufanikiwa kusawazisha bao dakika ya 48, mfungaji Nahodha wake, Thomas Batista kabla ya kufunga la pili dakika ya 60 mfungaji Bony Martin.

Atlabara ilipata pigo dakika ya 89 baada ya Nahodha wake, Batista kutolewa nje kwa kadi nyekundu. Kwa matokeo hayo, Azam inafikisha pointi tano baada ya mechi tatu na kujihakikishia nafasi ya kwenda Robo Fainali ya michuano hiyo, wakati Atlabara inafikisha pointi mbili baada ya mechi mbili.

Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Gardiel Michael, Shomary Kapombe, Said Mourad, Aggrey Morris, Kipre Balou, Himid Mao, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Gaudence Mwaikimba/Didier Kavumbangu dk63, Leonel Saint Preux na Kipre Tchetche/Khamis Mcha dk63. Atlabara; Jacko Mpenzi, Thomas Batista, Hamza Olema, Hatit Monydeng, Ibrahim Sebit, Kharim Mutawakil, Frando Justin Wani, Joseph Aquer, Dak Kujbor/Khamis Leon dk56 na Bony Martin.
   BONYEZA HAPA KUJINGA NA BLOG HII 

Tuesday, August 12, 2014

BAADA YA DIAMOND SASA NI ZAMU YA CINDY RULZ KUIWAKILISHA VYEMA BONGO KATIKA TUZO HUKO MAREKANI. SOMA HAPA

Baada ya kuepo uvumi wa mda mrefu kua msani Cindy Rulz anatoka kimapenzi na producer Lamar hatimaye Cindy mwenyewe ameamua kufunguka na kusema ukweli wote kuhusiana na ishu hiyo.

Cindy alisema kua Lamar ni kama kaka yake na kamwe hawezi kua na uhusiano nae kimpenzi. Cindy aliyasema hayo jana usiku wakati akihojiwa katika kipindi cha Ala za roho kinachorushwa na Clouds huku mtangazaji akiwa Diva Loveness Love.

Pia Diva alimuuliza kuhusu tetesi za Cindy kuachana mpenzi wake ( Gosby ) na Cindy alisema kuwa hajawahi kuachana na gosby maana kipindi cha nyumba inasemekana alimkuta gosby na wasichana wamemkumbatia wakiwa wanapiga picha so alikasirika akampiga kibao lakini alikiri licha ya kila mahusiano kuwa na matatizo yake.

Wamedumu kwa miaka 6 sasa katika mapenzi yao. Pia Cindy alipata nafasi ya kuwaomba mashabiki wake wote waweze kumpigia kura katika tuzo za Under Ground Music Awards zinazotolewa huko nchini Marekani.

Cindy alisema kua ataenda New York ambako ndipo tuzo hizo zinatolewa kwa ajili ya kuchukua tuzo hizo lakini akasisitiza kua watu anawaomba sana mashabiki wote waweze kumpigia kura.

Jinsi ya kumpigia kura tembelea website hii www.undergroundmusicawards.com na umpigie kura Cindy aliyechaguliwa katika kipengele cha Best African Artist.

Watu wanashauriwa to vote for her ili kumuwezesha kushinda.

 BONYEZA HAPA KUJIUNGA NASI 

DIAMOND UNAHITAJI PONGEZI KWA HIKI ULICHOKIFANYA KWA MSHINDI WA SUPER NYOTA MWANZA

Wakati msako wa kuwatafuta akina dada wanye vipaji vya kuimba kupitia Super Nyota Divas inayoendeshwa na Fetty kupitia Clouds FM ukiendelea katika mikoa mingine 17 baada ya kufanyika katika mkoa wa Mwanza, Diamond aahidi kufanya collable na mshindi wa Super Nyota Akiwa kwenye stage baada ya ku-perform na Lina "Kizaizai" Diamond alitoa tamko hilo akisema

 KAMA BADO UJAJIUNGA NA BLOG HII BONYA HAPA 

NISHER ACHANWA KWA KUSEMA UONGO KUMHUSU PRODUCER HUYU WA VIDEO.

Katika pitapita zangu leo Facebook nkakutana na post ya aliyekua muandaaji mwenza wa Nisher Director wa video za mziki hapa Bongo ikitoa ufafanuzi kuhusu alichokiandika Nisher katika ukurasa wake Facebook. Bamushka amesema kua alichokiandika Nisher ni uongo na huu ndo ukweli aliouandika Facebook

"NISHER WEWE HUKUNIFUNDISHA MIMI NNA ELIMU YANGU KUBWA TU YA PRODUCTION NA ULINIKUTA NAYO....FOR REAL IMESKITISHWA NA POST ZAKO ZOTE MBILI NILIAMUWA KUKAA KIMYA COZ MIMI NI MTU MZIMA NA NAJUWA NINI NAFANYA NA NAJUWA UWEZO WAKO WA KUFIKIRI UNAISHIA WAPI ... BUT NAONA STIL UNAENDELEA KUDANGANYA WATU KWA KUNICHAFUWA MIMI NIONEKANE NIME KU SNITCH...UKWELI NI KWAMBA SIWEZI FANYA KAZI ISIYO NA FAIDA MIMI NI MTU MZIMA NAHITAJI KU RUN MAISHA YANGU KUPITIA KILE NNACHOKIFANYA ASA KAMA HAKUNA MASLAHI KWANINI NIENDELEE KUWA UNDER YOU? ( sifanyi kazi isiyo na faida ) .... THEN VIDEI ZOTE ULIZO ZITAJA HAPO JUU WEWE HUKUHUSIKA HATA KIDOGO YANI HATA KIDOGO HIZO VIDEO HAZIPO UNDER N.E HIZO ZIPO UNDER ME...MPAKA ZINAFIKA INTERNATIONAL LEVEL U JUST KNOW NOTHING ABOUT IT IS JUT MY OWN POWER...ZINGAITIA HAKUNA ULICHONIFUNDISHA BUT TUMEFUNDISHANA...WEWE HUJANIFUNDISHA WAPO WALIONIFUNDISHA NA WAMEKAA KIMYA... KAMA UMENIFUNDISHA HEBU FANANISHA VIDEO YA CHIN BINZ - LET ME KNOW NA YA LUCCI - SUMU ZOTE NI WHITE SCREEN NA TULITOA AT THE SAME TIME...HIVI NI VIDEO YANGU GANI WE USHAWAHI KUJA LOCATION KAZI YA HIZO ULIZOZITAJA HAPO JUU?... ME SIWEZI LOST A DAYS KUFANYA KAZI ISYONIINGIZIA PESA COZ MIMI SIO KAMA WEWE UKIRUDI HOME UNAKUTA FOOD ON THE TABLE..MEN I DO MY OWN HUSTLING NAHITAJI FIGHT FOR MA OWN...SOO MIMI KUACHA KUFANYA KAZI NA WEWE ISIKUUME KIASI CHA KUKESHA UNA POST POST SHIT ABOUT ME...UKWELI NI KWAMBA NAHITAJI FANYA MISHE ZANGU AU WEWE HUPENDI MIMI NIKIFANIKIWA ? SOMETIMES ETI UNANIKATAZA NISIPIGE STORY NA HIVI WE UNAJUWA ME NA HUYU JAMAA TUMETOKA FAR KIASI GANI ?...MEN ME SIO DIRECTOR WA FACEBOOK WALA INSTAGRAM KAMA WEWE...NYAMAZA LET WORK MAKE NOISE...KUWA MWANAUME SOMETIMES ... AM DONE ... 1 COPPY TO DIRECTOR HANSCANA NA WOTE WANAOTUFAHAMU SINCE DAY 1" Hanscana dE Lavenche Minzi Mims Jozeey Joseph Adam Shani Shine Ande John Cyrill Kamikaze G- The Navigator George Laurent F J Kimbatu Jimmy Cooge Guru G-lover Nisher nae aliandika kua

"Nisher Entertainment Inasikitika kuwataarifu Wadau wake wote na Mashabiki wote wa kazi zetu Kua hatakua Akifanya kazi pamoja nasi Tena! Khalfani Bamushka Ni kama mwaka na Nusu sasa NISHER (C.E.O and President wa NISHER ENTERTAINMENT) Ali-gundua Kipaji Cha khalfani kwa njia ya facebook.. na baada ya hapo walikutana na kuanza kufanya kazi pamoja... Khalfani amejifunza Mengi Kuhusu Video Production Kutoka kwa Mshindi wa Tuzo Za watu 2014 Director Nisher, katika kipindi chote alichokaa kwa karibu sana na Nisher. Khalfani aliweza pia kupata nafasi ya kufanya videos alizozioongoza yeye mwenyewe Chini ya Nisher Entertainment kama "LET ME KNOW" ya iliyo pata kuchezwa Channel O...., pamoja na Video Mpya Ya Baby Madaha, Pamoja na Kazi Nyinginezo Nyingi ambazo zilimwezesha Kupata Jina na Kujiweka vizuri zaidi katika Uongozaji na Uandaaji wa Videos.

Nisher Entertainment Pamoja na C.E.O. wake Tunatambua Juhudi na Bidii aliyokua nayo Khalfani na Tunamshukuru Kwa Mchango wake Katika Kufanikisha Shughuli zote za Nisher Entertainment.

Mwisho....Nisher Entertainment inaendelea kufanya Msako wa Vipaji mbali mbali ili kuwapa Ajira vijana wetu kupitia Mitandao ya kijamii... hivyo wadau wote na wote wale wanao penda kazi zao zionekane Msiache kuzituma kwenye inbox yetu....Tunawashukuru kwa kuendelea ku- Support kazi zetu! Ahsanteni.

NISHER ENTERTAINMENT"

Mganga wa Jadi Aua mgonjwa wake kwa kumtandika fimbo kichwani wakati Akimtibu

Kijana mmoja aliyejulikana kwa jina la Vicent Kawawa (28) ameuawa kwa kupigwa na fimbo na kitu kizito kichwani na mganga wa kienyeji aliyekuwa anamtibu ugonjwa wa akili nyumbani kwake katika kijiji cha Buduba kata ya Nyandekwa wilayani Kahama mkoani Shinyanga.

Kamanda wa jeshi la polisi mkoa wa Shinyanga SACP Justus Kamugisha alisema tukio hilo limetokea Agosti 5 mwaka huu saa 12 jioni.

Alisema Vicent Kawawa(28) mkazi wa kijiji cha Buduba akiwa nyumbani kwa mganga wa jadi aitwaye Mihayo Isheli akitibiwa ugonjwa wa akili aliuawa kwa kupigwa na fimbo na kitu kizito kichwani na mganga huyo na watu waliokuwepo eneo la tukio na kusababisha kifo chake papo hapo.

Kamanda Kamugisha alisema chanzo cha tukio hilo ni kwamba mgonjwa alipandisha kichaa na kuanza kumpiga mganga wa jadi na watu waliokuwa eneo hilo na ndipo katika kumtuliza mganga alianza kumpiga akisaidiwa na watu hao ambao idadi yao haijajulikani na kusababisha kifo chake papo hapo.

Alisema baada ya tukio hilo mganga Mihayo Isheli alikimbia na familia yake pamoja na watu waliokuwa katika eneo hilo na kwamba jeshi la polisi linaendelea na uchunguzi sambamba na kumtafuta mganga huyo na wahusika wengine waliokuwa katika eneo la tukio.

By mdadisiblog/festo saimon

 KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BONYA HAPA ILI KILA HABARI TUPATAPO ZIKUFIKIE KIRAHISI 

Van Gaal awaonyesha Chicharito, Nani mlango wa kutokea Man United

Na festo saimon SIKU chache kabla ya kuanza kwa Ligi Kuu ya England na kufungwa kwa pazia la usajili katikia ligi hiyo, Kocha wa Manchester United, Louis van Gaal amewaeleza wachezaji sita akiwamo beki wa kulia Rafael kwamba wanaweza kuchapa mwendo. Marouane Fellaini, Wilfried Zaha, Nani, Shinji Kagawa na kinda yosso Will Keane pia wamevunja 'ndoa' na kikosi hicho cha Van Gaal na hilo limefanyika wakati United ikijifua katika Uwanja wa mazoezi wa Carrington Jumamosi mchana.

Inaeleweka kuwa Mholanzi huyo amewaambia Fellaini, Zaha, Nani na Keane klabu hiyo itasikiliza ofa kwao baada ya kuwaweka sokoni rasmi.

Rafael, alishangaa kusikia jina lake likiwa katika orodha hiyo na kwamba pia anaweza kulazimisha kuondoka wakati huu klabu hiyo ikisaka beki wa kulia.

Kagawa atatumika lakini kaelezwa ataanzia benchi nyuma ya Ander Herrera na Juan Mata. Kiungo Anderson na mshambuliaji Javier Hernandez pia nao tayari wanajua kwamba United itasikiliza ofa endapo zitawasili mezani kwao.

Southampton, Inter Milan, Tottenham, Atletico Madrid na Juventus zote zimeonyesha nia ya kumsajili Mmexico huyo, wakati Napoli itakuwa tayari kumsajili Fellaini kama dili hilo litakubalika na United.

Newcastle inaongoza katika vita ya kumsajili Zaha, huku Crystal Palace, West Ham na Nottingham Forest nazo zikihitaji huduma yake.

Cardiff City imeulizia uwezekano wa kumsajili kwa mkopo Keane ambaye ni pacha wa beki Michael, lakini United inahitaji kumtazama zaidi kabla ya kukamilisha dili hilo.
Kwa sasa United ipo sokoni ikisaka mabeki wapya wawili baada ya kushindwa kumsajili beki wa kati wa Arsenal, Thomas Vermaelen ambaye juzi alijiunga rasmi na Barcelona Mabingwa hao wa zamani wamejipanga kufanya vyema katika msimu huu baada ya msimu uliopita kuboronga na kumaliza kwenye nafasi ya katikati tofauti na mazoea yao.

 KAMA BADO UJAJIUNGA NA BLOG HII YA MDADISI BONYA HAPA 

KWA HILI WEMA SEPETU UNAISHUSHA HADHI YAKO YA KUWA MKE WA DIAMOND PLATNUMZ

Mara nyingi Wema amekuwa akimsupport mchumba wake kwa kupanda naye jukwaani na hivyo kusababisha shangwe kubwa.

ushabiki wa Wema kwa Diamond kidogo umepitiliza na hata kama umekuwa ukishangiliwa, tunahisi anajishusha kiaina.

Kuna ile hadhi ya mke lazima ilindwe hasa kama mke ama mpenzi wako si msanii kama wewe.

Wema ni muigizaji si dancer ama mwanamuziki na kwa muigizaji wa filamu mwenye mashabiki wengi, kupanda jukwaani na kukata viuno design kama ni kushusha brand ama nini? Si mbaya kama angekuwa akipanda na kutoa salamu fupi kisha kushuka na kuwa mtazamaji kama watu wengine. Tupe Mtazamo wako
 BONYEZA HAPA 

HABARI MBAYA KWA MASHABIKI WA LADY JAYDEE, YADAIWA NDOA YAKE NA GARDNER YAVUNJIKA.

Ndoa ya mwanuziki Jay dee na mtangazaji mashuhuri wa radio Gardner G. Habash inasemekana imevunjika huku Gardner akihama Kimara alikokua akiishi na mkewe na kuhamia kwa moja wa ndugu zake wa karibu sana.

chanzo cha kuvunjika ndoa hiyo bado hakijajulikana moja moja kwa moja ila wawili hao wamekuwa katika migogoro kwa muda.. na si mara ya kwanza kutengana ila this time hali si shwari. yazidi kusemekana kaka Gardner kazidi michepuko amekua haibi tena anafanya bayana mpaka mwenye mali anajua anavyoibiwa.

kudhihirisha hayo katika ukurasa wake wa IG dada jide ameandika "Walking Away From Troubles" ambapo umbepuzi yakinifu waonesha mambo si sawa hata kidogo. Gardner kabla ya kumuoa Jide alikua tayari na mke halali wa ndoa na mtoto mmoja.

 BONYEZA HAPA KAMA BADO UJAJIUNGA NASI  

TETESI ZA SOKA ZILIZOSHAMILI KWENYE MAGAZETI MBALIMBALI YA ULAYA LEO JUMANNE ZIPO HAPA

Beki wa Liverpool Kolo Toure, 33, anajiandaa kujiunga na Trabzonspor ya Uturuki katika mkataba wa pauni milioni 1.5 (Daily Mail), boss wa Liverpool Brendan Rodgers anafikiria kumchukua mshambuliaji kutoka Cameroon, Samuel Eto'o, 33, ambaye ni mchezaji huru baada ya kuondoka Chelsea msimu uliopita (Guardian), Galatasaray wanafikiria kutoa pauni milioni 28 kuwachukua Joel Campbell, 22, na Lukas Podolski, 29, kutoka Arsenal (Daily Express), QPR wapo tayari kumtoa Loic Remy, 27, kubadilishana na Andros Townsend, 23, na Harry Kane, 21 kutoka Tottenham (CaughtOffside), Remy pia huenda akawindwa na Chelsea, wakati Jose Mourinho akitafuta mchezaji wa kuziba pengo la Didier Drogba, 36, aliyeumia (Goal), kiungo kutoka Spain Santi Cazorla, 29, ametupilia mbali tetesi kuwa anataka kuondoka Arsenal na kurejea La Liga (Daily Mirror), Stoke City wamepanda dau jipya na kutoa pauni milioni 5 kutaka kumchukua winga wa Norwich Nathan Redmond, 20 (Daily Mail), Aston Villa wanakaribia kumchukua Carlos Sanchez, 28, kwa pauni milioni 3.5 (Birmingham Mail), mshambuliaji wa Chelsea Didier Drogba huenda asiweze kucheza kwa miezi minne baada ya kuumia 'enka' katika mchezo wa kirafiki dhidi ya Ferencvaros (Daily Mirror), Southampton huenda wakampiga faini Morgan Schneiderlin, 24, iwapo kiungo huyo Mfaransa atakataa kucheza mechi ya Ligi Kuu ya England dhidi ya Liverpool siku ya Jumapili (Daily Telegraph), kipa wa Manchester City Willy Caballero, 32 amemwambia kipa mwenzake Joe Hart, 27, atalazimika kupigania namba moja, Etihad (Telegraph), Chelsea wanamfuatilia beki wa kati wa Roma, Mehdi Benatia, 27, ambaye anadhaniwa kuwa na thamani ya pauni milioni 30 (Daily Mirror), Arsenal wanafikiria kutoa pauni milioni 10 kumshawishi beki wa kati wa Liverpool Daniel Agger (The Sun), Everton na Tottenham wako 'macho' baada ya kuambiwa Salomon Kalou anaweza kuondoka Lille kabla ya dirisha la usajili kufungwa (Daily Mirror), Arsenal wapo tayari kumfuatilia beki wa Olympiakos Kostas Manolas kuziba pengo la Thomas Vermaelen aliyekwenda Barcelona (Daily Express).

 KAMA BADO UJAUNGANA NASI BONYEZA HAPA 

BREAKING NEWS: DEREVA WA BASI LA WACHEZAJI WA YANGA AFARIKI DUNIA ASUBUHI HII

Uongozi wa klabu ya Young Africans unasikitika kutangaza kifo cha aliyekuwa Dereva wa Bus Kubwa la Wachezaji (Yutong) Bw Maulid Kiula kilichotokea alfajiri ya leo Ilala jijini Dar es salaam.

Taratibu za mazishi zinaendelea nyumbani kwa marehemu mtaa wa Chunya karibu na Bungoni Ilala jijini Dar es salaam.

Mwenyezi Mungu aiweke roho ya marehemu mahali pema peponi

MUHIMU SANA: USAILI WA JESHI LA POLISI TANZANIA KWA WAKAZI WA MBEYA

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya, BARAKAEL .N. MASAKI – ACP anawatangazia Wananchi wote ya kuwa orodha ya majina ya vijana waliomaliza Kidato cha Nne mwaka 2013 na cha Sita mwaka 2014 na kuchaguliwa kufanya usalii wa kujiunga na Jeshi la Polisi inapatikana kwenye tovuti ya Polisi: www.policeforce.go.tz au wafike ofisi ya kamanda wa Polisi mkoa wa Mbeya iliyopo Forest jirani na Mahakama kuangalia majina yao.

Muhimu:

• Mwombaji anaruhusiwa kufanya usaili kwenye kituo chochote cha usaili kilicho karibu naye kulingana na tarehe zinavyoonesha kwenye jedwali hapo juu ili mradi tu awe amejiridhisha kuwa ni miongoni mwa walioitwa kwenye usaili. Jeshi la Polisi halitahusika na lawama yoyote ile kwa mtu atakayekwenda kwenye kituo cha usaili hali ambapo jina lake si miongoni mwa walioitwa kufanya usaili.

• Mwombaji aliyeitwa kwenye usaili aje na vyeti vyake vyote vya masomo [(Academic Certificate(s)/Results slip(s) & Leaving certificate(s) ], nakala halisi ya cheti cha kuzaliwa (Original Birth certificate). Hati ya kiapo cha kuzaliwa haitakubalika.

• Mwombaji awe na namba ya simu itakayotumika kumjulisha endapo atachaguliwa..

• Kila mwombaji aliyeitwa kwenye usaili atajigharamia usafiri, chakula na malazi kwa muda wote wa zoezi la usaili. Pia waombaji waje na kalamu za wino kwa ajili ya usaili wa kuandika.

Ni muhimu sana kwa kila mwombaji kuzingatia muda wa kuanza usaili.

TAREHE YA USAILI KWA MKOA WA MBEYA NI 28.09.2014 HADI
01.10.2014. SAA 08:00 ASUBUHI HADI 10:00 JIONI.

Na mdadisiblog/festo saimon

 BONYEZA HAPA KAMA BADO UJAJIUNGA NASI 

Mkali wa movie Robin William akutwa amefariki ndani ya nyumba yake

Robin William ni star aliyeanza kupata mafanikio akifanya kazi kama stand up comedian na baadae kuanza kuonekana kwenye movie.

Akiwa na miaka 63 Robin amefariki dunia kwa kifo ambacho hadi sasa hakijajulikana chanzo chake lakini tetesi zinasema kuna uwezekanao kwamba Robin alijiua.

Mwili wake umekutwa nyumbani kwake huko Tiburon California na watu wa karibu wanasema alikuwa anasumbuliwa na msongo wa mawazo hivi karibuni.

Enzi za uhai wake aliwai kushiriki kwenye movie kama The Fisher King,Good will Hunting,Jumanji,Popeye na nyingine. Pia alishinda tuzo kama Academy,Golden Globe,Emmy,Grammy na nyinginezo kwa wakati tofauti.

 KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BONYEZA HAPA 

Huu ndiyo usajili wa timu za Ligi Kuu za England

Romelu Lukaku amehamia jumla Everton toka Chelsea
Fillipe Luis (mbele) amehamia Chelsea
Didier Drogba amerejea Chelsea
Kipa David Ospina ametua Arsenal
Luke Shaw ametua Manchester United toka Southampton
Alexis Sanchez ametua Arsenal toka Barcelona

ARSENAL
WALIOSAJILIWA
Alexis Sanchez (Barcelona, £30m),
Calum Chambers (Southampton, £12m),
Mathieu Debuchy (Newcastle, £10m),
David Ospina (Nice, £3m)

WALIOONDOKA
Thomas Eisfeld (Fulham, ada haikutajwa),
Bacary Sagna (Manchester City, huru),
Lukasz Fabianski (Swansea, huru),
Nicklas Bendtner (ameruhusiwa),
Park Chu-young (ameruhusiwa),
Chuks Aneke (ameruhusiwa),
Daniel Boateng (ameruhusiwa),
Wellington Silva (Almeria, mkopo),
Carl Jenkinson (West Ham, mkopo)

ASTON VILLA
WALIOSAJILIWA
Philippe Senderos (Fulham, huru),
Joe Cole (West Ham, huru),
Tom Leggett (Southampton, ada haikutajwa),
Isaac Nehemie (Southampton, ada haikutajwa)
Kieran Richardson (Fulham, ada haikutajwa)

WALIOONDOKA
Marc Albrighton (Leicester City, huru),
Nathan Delfouneso (Blackpool, huru),
Jordan Bowery (Rotherham, ada haikutajwa),
Nicklas Helenius (Aalborg, mkopo),
Yacouba Sylla (Kayseri Erciyesspor, mkopo)

BURNLEY
WALIOSAJILIWA
Lukas Jutkiewicz (Middlesbrough, £2.5m),
Michael Kightly (Stoke, ada haikutajwa),
Marvin Sordell (Bolton, huru),
Matt Gilks (Blackpool, huru),
Matt Taylor (West Ham, huru),
Steven Reid (West Brom, huru)

WALIOONDOKA
Chirs Baird (West Brom, huru),
Junior Stanislas (Bournemouth, huru),
David Edgar (Birmingham, huru),
Keith Treacy (ameruhusiwa),
Brian Stock (ameruhusiwa),
Nick Liversedge (ameruhusiwa)

CHELSEA
WALIOSAJILIWA
Cesc Fabregas (Barcelona, £30m),
Diego Costa (Atletico Mdrid, £32m),
Mario Pasalic (Hadjuk Split, ada haikutajwa),
Filipe Luis (Atletico, £16m),
Didier Drogba (Galatasaray, huru)

WALIOONDOKA
David Luiz (Paris Saint-Germain, £50m),
Romelu Lukaku (Everton, £28million),
Samuel Eto'o (ameruhusiwa),
Frank Lampard (New York City, huru),
Sam Hutchinson (Sheffield Wednesday, huru),
Mark Schwarzer (ameruhusiwa),
Henrique Hilario (ameruhusiwa),
Wallace (Vitesse Arnhem, mkopo),
Bertrand Traore (Vitesse Arnhem, mkopo)
Thorgan Hazard (Borussia Monchengladbach, mkopo),
Ashley Cole (Roma, £1.5m),
Demba Ba (Besiktas, £8m),
Mario Pasalic (Elche, mkopo)
Patrick van Aanholt (Sunderland, ada haikutajwa),
Ryan Bertrand (Southampton, mkopo),
Gael Kakuta (Rayo Vallecano, mkopo)

CRYSTAL PALACE
WALIOSAJILIWA
Chris Kettings (Blackpool, huru)
Fraizer Campbell (Cardiff, £800k)

WALIOONDOKA
Jonathan Parr (Ipswich, huru),
Dean Moxey (Bolton, huru),
Aaron Wilbraham (Bristol City, huru),
Kagisho Dikgacoi (Cardiff, huru),
Danny Gabbidon (ameruhusiwa),
Neil Alexander (ameruhusiwa),
Ibra Sekajja (ameruhusiwa),
Alex Wynter (Portsmouth, mkopo),
Kwesi Appiah (Cambridge, mkopo),
Jose Campana (Sampdoria, ada haikutajwa),
Jack Hunt (Nottingham Forest, mkopo)

EVERTON
WALIOSAJILIWA
Romelu Lukaku (Chelsea, £28m),
Gareth Barry (Manchester City, free)
Muhamed Besic (Ferencvaros, £4m)

WALIOONDOKA
Apostolos Vellios, (Lierse, huru)
Mason Springthorpe (ameruhusiwa)
Magaye Gueye (Millwall, huru)

HULL
WALIOSAJILIWA
Robert Snodgrass (Norwich, £8m),
Jake Livermore (Tottenham, £6m),
Tom Ince (Blackpool, free),
Harry Maguire (Sheffield United, £2.5m),
Andrew Robertson (Dundee United, £2.85m)

WALIOONDOKA
Matty Fryatt (Nottingham Forest, huru),
Cameron Stewart (Ipswich, huru),
Robert Koren (ameruhusiwa),
Abdoulaye Faye (ameruhusiwa),
Conor Henderson (Crawley, huru),
Dougie Wilson (released),
Conor Townsend (Dundee United, mkopo),
Joe Dudgeon (Barnsley, mkopo)

LEICESTER CITY
WALIOSAJILIWA
Matthew Upson (Brighton, huru),
Marc Albrighton (Aston Villa, huru),
Leonardo Ulloa (Brighton, £7m),
Ben Hamer (Charlton, huru),
Jack Barmby (Manchester United, huru),
Louis Rowley (Manchester United, huru)

WALIOONDOKA
Lloyd Dyer (Watford, huru),
Neil Danns (Bolton, huru),
Sean St Ledger (ameruhusiwa),
Zak Whitbread (Derby, huru),
Paul Gallagher (Preston, mkopo),
Marko Futacs (ameruhusiwa),
George Taft (Burton Albion, huru)

LIVERPOOL
WALIOSAJILIWA
Adam Lallana (Southampton, £23m),
WALIOONDOKA
Luis Suarez (Barcelona, £75m),
Luis Alberto (Malaga, mkopo),
Iago Aspas (Sevilla, mkopo),
Andre Wisdom (West Brom, mkopo),
Divock Origi (Lille, mkopo)

MANCHESTER CITY
WALIOSAJILIWA
Fernando (Porto, £12m),
Bacary Sagna (Arsenal, free),
Willy Caballero (Malaga, £6m),
Bruno Zuculini (Racing Club, £1.5m)

WALIOONDOKA
Costel Pantilimon (Sunderland, huru),
Joleon Lescott (West Brom, huru)
Gareth Barry (Everton, huru),
Alex Nimely (ameruhusiwa),
Rony Lopes (Lille, mkopo),
Emyr Huws (Wigan, mkopo)

MANCHESTER UNITED
WALIOSAJILIWA
Luke Shaw (Southampton, £31.5m),
Ander Herrera (Athletic Bilbao, £29m),
Vanja Milinkovic (FK Vojvodina, ada haikutajwa)

WALIOONDOKA
Alexander Buttner (Dinamo Moscow, £5.6m),
Rio Ferdinand (QPR, huru),
Nemanja Vidic (Inter Milan, huru),
Federico Macheda (Cardiff City, huru),
Jack Barmby (Leicester, huru),
Louis Rowley (Leicester, huru)
Ryan Giggs (amestaafu),
Patrice Evra (Juventus, £2.5m)
Bebe (Benfica, £2.4m)

NEWCASTLE
WALIOSAJILIWA
Remy Cabella (Montpellier, £12m),
Emmanuel Riviere (Monaco, £6m),
Siem de Jong (Ajax, £6m),
Daryl Janmaat (Feyenoord, £5m),
Ayoze Perez (Tenerife, £1.5m),
Jack Colback (Sunderland, huru)

WALIOONDOKA
Mathieu Debuchy (Arsenal, £10m),
James Tavernier (Wigan, ada haikutajwa,
Dan Gosling (Bournemouth, huru),
Shola Ameobi (ameruhusiwa),
Conor Newton (Rotherham, huru),
Michael Richardson (ameruhusiwa),
Sylvain Marveaux (Guingamp, mkopo)

QUEENS PARK RANGERS
WALIOSAJILIWA
Rio Ferdinand (Manchester United, huru),
Steven Caukler (Cardiff, £8m)

WALIOONDOKA
Tom Hitchcock (Mk Dons, huru),
Aaron Hughes (Brighton, huru)
Stephane Mbia (ameruhusiwa),
Andrew Johnson (ameruhusiwa),
Luke Young (ameruhusiwa),
Hogan Ephraim (ameruhusiwa),
Angelo Balanta (ameruhusiwa),
Yossi Benayoun (Maccabi Haifa, ada haikutajwa),
Esteban Granero (Real Sociedad, ada haikutajwa)

SOUTHAMPTON
WALIOSAJILIWA
Dusan Tadic (Twente, £10.3m),
Graziano Pelle (Feyenoord, £8m),
Ryan Bertrand (Chelsea, loan)

WALIOONDOKA
Luke Shaw (Manchester United, £31.5m),
Rickie Lambert (Liverpool, £4m),
Adam Lallana (Liverpool, £23m)
Guly do Prado (released),
Lee Barnard (Southend, huru),
Jonathan Forte (released),
Danny Fox (Nottingham Forest, huru),
Andy Robinson (Bolton, huru),
Tom Leggett (Aston Villa, ada haikutajwa),
Isaac Nehemie (Aston Villa, ada haikutajwa)
Dejan Lovren (Liverpool, £20m)
Calum Chambers (Arsenal, £12m)

STOKE CITY
WALIOSAJILIWA
Mame Biram Diouf (Hannover, huru),
Dionatan Teixeira (Banska Bystrica, ada haikutajwa),
Phil Bardsley (Sunderland, huru),
Steve Sidwell (Fulham, huru),
Bojan Krkic (Barcelona, ada haikutajwa)

WALIOONDOKA
Michael Kightly (Burnley, ada haikutajwa),
Matthew Etherington (ada haikutajwa),
Juan Agudelo (ada haikutajwa)

SUNDERLAND
WALIOSAJILIWA
Billy Jones (West Brom, huru),
Jordi Gomez (Wigan, huru),
Costel Pantilimon (Manchester City, huru)
Patrick van Aanholt (Chelsea, ada haikutajwa)

WALIOONDOKA
Jack Colback (Newcastle, huru),
Craig Gardner (West Brom, huru),
Phil Bardsley (Stoke, huru),
Billy Knott (Bradford, huru)
Keiren Westwood (Sheffield Wednesday, huru),
Carlos Cuellar (ameruhusiwa),
Andrea Dossena (ameruhusiwa),
Louis Laing (ameruhusiwa),
Oscar Ustari (Newell's, huru),
David Vaughan (Nottingham Forest, huru),
John Egan (Gillingham, huru),
Ignacio Scocco (Newell's, £800,000)

SWANSEA
WALIOSAJILIWA
Marvin Emnes (Middlesbrough, £1.5m),
Bafetimbi Gomis (Lyon, huru),
Lukasz Fabianski (Arsenal, huru),
Stephen Kingsley (Falkirk, ada haikutajwa),
Gylfi Sigurdsson (Tottenham, ada haikutajwa)
Jefferson Montero (Monarcas Morelia, £4m)

WALIOONDOKA
Leroy Lita (ameruhusiwa),
David Ngog (ameruhusiwa),
Daniel Alfei (Northampton, mkopo),
Jernade Meade (ameruhusiwa),
Darnel Situ (ameruhusiwa),
Michu (Napoli, mkopo),
Ben Davies (Tottenham, £10m)
Michel Vorm (Tottenham, £5m)
Alejandro Pozuelo (Rayo Vallecano, ada haikutajwa)

TOTTENHAM
WALIOSAJILIWA
Ben Davies (Swansea, ada haikutajwa Lazar Markovic WALIOONDOKA
Jake Livermore (Hull, £6m),
Heurelho Gomes (Watford, huru),
Cameron Lancaster (ameruhusiwa),
Alex Pritchard (Brentford, mkopo),
Gylfi Sigurdsson (Swansea, mkopo)

WEST BROMWICH ALBION
WALIOSAJILIWA
Brown Ideye (Dynamo Kiev, £10m),
Craig Gardner (Sunderland, huru),
Joleon Lescott (Manchester City, huru),
Chris Baird (Burnley, huru),
Sebastien Pocognoli (Hannover 96, ada haikutajwa),
Andre Wisdom (Liverpool, mkopo)

WALIOONDOKA
Liam Ridgewell (Portland Timbers, huru),
Billy Jones (Sunderland, huru),
Steven Reid (Burnley, huru),
Cameron Gayle (Shrewsbury, huru),
Diego Lugano (ameruhusiwa),
Zoltan Gera (ameruhusiwa),
Scott Allan (ameruhusiwa),
Nicolas Anelka (ameruhusiwa),
George Thorne (Derby County, ada haikutajwa)

WEST HAM
WALIOSAJILIWA
Enner Valencia (Pachuca, £12m),
Cheikhou Kouyate (Anderlecht, £7m),
Mauro Zarate (Velez Sarsfield, ada haikutajwa),
Aaron Cresswell (Ipswich, ada haikutajwa),
Diego Poyet (Charlton, ada haikutajwa),
Carl Jenkinson (Arsenal, huru)

WALIOONDOKA
Joe Cole (Aston Villa, huru),
Matt Taylor (Burnley, huru),
Stephen Henderson (Charlton, huru),
Jack Collison (ameruhusiwa),
George McCartney (ameruhusiwa),
Callum Driver (ameruhusiwa),
Jordan Spence (ameruhusiwa), (Benfica, £20m),
Emre Can (Bayer Leverkusen, £9.8m),
Rickie Lambert (Southampton,

By mdadisiblog/festo saimon

 KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BONYA HAPA ILI KILA NIKIPATA HABARI ZIKUFIKIE KIRAHISI 

MARADONA AMCHAPA KIBAO MWANDISHI WA HABARI.

Gwiji la soka ulimwenguni Diego Maradona ameibuka na skendo nyingine nchini Argentina baada ya kumzaba kibao mwandishi mmoja wa habari ambaye inasemekana alimsemea maneneo machafu mke wa zamani wa gwiji huyo. Kitrndo hicho kilimuhudhi Maradona ambaye alikuwa safarini pamoja na mtoto wake.

 ASANTE NA KALIBU TENA ILA KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BONYA HAPA 

DIAMOND PLATNUM- ”MRISHO NGASSA NDIYE MWANASOKA PEKEE NINAYEMFAHAMU TANZANIA”

Mwanamuziki wa Bongo Flovour Nchini Nasib Abdul maarufu kama Diamond Platinums, amesema hajaridhilika na alipo sasa kimuziki, ndio maana kila siku anajifunza kwa kufuatilia kwa ukaribu maisha ya Nyota wengi hasa wanamichezo Kutoka Mataifa Tofauti Duniani.

Diamond ambae ni miongoni mwa wanamuziki waliofanya vyema kwenye jukwaa la Serengeti Fiesta Mkoani Mwanza hivi karibuni, ametoa taarifa za kuwafuatilia nyota hao mbalimbali kwenye mahojiano maalum na Shaffih Dauda, kupitia Dauda TV. Miongoni mwa nyota ambao Diamond anawafuatilia hasa kupitia Mtandao wa Instagram, ni Mshambuliaji wa Timu ya Taifa ya Cameroon Samuel Etoo, Kiungo Mshambuliaji wa Brazil na Barcelona Neymar, Bondia Mmarekani Floyd Myweather na wengineo.

Pamoja na Diamond kuweka hilo wazi, pia amesema aliwahi kucheza masumbwi, kisha akahamia kwenye Soka hasa nafasi ya golikipa na namba sita yaani kiungo Mkabaji, lakini aliamua kuachana na Soka baada ya mama yake kumsii kufanya hivyo kwa muda mrefu.

Awali kulikuwa na hisia kwamba Diamond anashabikia timu ya Dar-es- salaam Young Africans, hasa baada ya kuweka picha kwenye mitandao akiwa na Mrisho Ngasa mara kadhaa, lakini amesema yeye na Ngasa ni marafiki, na sio mshabiki wa Yanga kama inavyodhaniwa.

Diamond ameongeza kwa kusema sio tu haishabikii Yanga, bali kwa hapa nyumbani hana timu anayoishabikia, badala yake anaipenda FC Barcelona ya Hispania, ambapo amesema kunakipindi mapenzi yalizidi kwa timu hiyo, kiasi cha kuweza kupanga kikosi chote.

 BONYEZA HAPA KUHUNGANA NASI ILI KILA TUKIPATA HABARI ZIKUFIKIE KIRAHISI 

Credit: dauda