Wednesday, August 13, 2014

RONALDO APIGA ZOTE MBILI REAL MADRID IKIUA 2-0 NA KUTWAA NDOO KUBWA KULIKO ZOTE ZA UEFA

Wafalme wa Ulaya; Wachezaji wa Real Madrid wakifurahia na taji lao la Super Cup ya UEFA leo
Magalactico wapya: Kikosi kipya cha kwanza cha Real Madrid kilichotwaa Super Cup leo
Mambo safi kabisa: Cristiano Ronaldo akishangilia baada ya kuifungia Real Madrid Uwanja wa Cardiff City

MABAO mawili ya Cristiano Ronaldo, moja kila kipindi yametosha kuipa Real Madrid ushindi wa 2-0 dhidi ya Sevilla, zote za Hispania Uwanja wa Cardiff City mjini Cardiff na kutwaa Super Cup ya UEFA. Sifa zimuendee nyota wa Wales, Gareth Bale aling'ara akicheza kwenye ardhi ya nyumbani na kutoa mchango mkubwa katika ushimdi huo.

Ronaldo alifunga bao la kwanza dakika ya 30 na la pili dakika ya 49. Kikosi cha Real Madrid kilikuwa: Casillas, Carvajal, Pepe, Sergio Ramos, Fabio Coentrao, Kroos, Rodriguez, Modric, Bale, Benzema, Ronaldo. Sevilla: Beto, Coke, Pareja, Fazio, Fernando Navarro, Alex Vidal, Krychowiak, Carrico, Vitolo, Suarez, Bacca.

 KAMA WEWE UNAPENDA USIPITWE NA HABARI MBALIMBALI ZA KIMICHEZO BONYA HAPA 

Credit binzubery

0 comments:

Post a Comment