Baada ya kuepo uvumi wa mda mrefu kua msani Cindy Rulz anatoka kimapenzi na producer Lamar hatimaye Cindy mwenyewe ameamua kufunguka na kusema ukweli wote kuhusiana na ishu hiyo.
Cindy alisema kua Lamar ni kama kaka yake na kamwe hawezi kua na uhusiano nae kimpenzi. Cindy aliyasema hayo jana usiku wakati akihojiwa katika kipindi cha Ala za roho kinachorushwa na Clouds huku mtangazaji akiwa Diva Loveness Love.
Pia Diva alimuuliza kuhusu tetesi za Cindy kuachana mpenzi wake ( Gosby ) na Cindy alisema kuwa hajawahi kuachana na gosby maana kipindi cha nyumba inasemekana alimkuta gosby na wasichana wamemkumbatia wakiwa wanapiga picha so alikasirika akampiga kibao lakini alikiri licha ya kila mahusiano kuwa na matatizo yake.
Wamedumu kwa miaka 6 sasa katika mapenzi yao. Pia Cindy alipata nafasi ya kuwaomba mashabiki wake wote waweze kumpigia kura katika tuzo za Under Ground Music Awards zinazotolewa huko nchini Marekani.
Cindy alisema kua ataenda New York ambako ndipo tuzo hizo zinatolewa kwa ajili ya kuchukua tuzo hizo lakini akasisitiza kua watu anawaomba sana mashabiki wote waweze kumpigia kura.
Jinsi ya kumpigia kura tembelea website hii www.undergroundmusicawards.com na umpigie kura Cindy aliyechaguliwa katika kipengele cha Best African Artist.
Watu wanashauriwa to vote for her ili kumuwezesha kushinda.
0 comments:
Post a Comment