Tuesday, August 26, 2014

Download new audio Abdu Kiba - Kabibi

 BOFYA HAPA  kudownload

Muziki unalipa: Davido anunua private Jet (ndege)yake icheki hapa

Mwimbaji wa ‘Ayee’ Davido wa Nigeria amethibitisha kuwa mbali na kuwa mtoto wa bilionea lakini muziki unamlipa kwa kiasi cha kumuwezesha kumiliki private Jet yake. Kama wewe unamfollow Davido kwenye Instagram yake bila shaka utakuwa shahidi kuwa ‘Skelewu’ hit maker anapiga show nyingi sana sababu post zake nyingi huwa ni kuhusu safari za show. Weekend iliyopita alipost picha akiwa kwenye private Jet hiyo kabla ya safari ya kuelekea Togo kwenye show nyingine.

SASA SIMBA WAIKEJELI VIBAYA SANA YANGA

VIONGOZI wa Simba wameiangalia Yanga katika mechi yao ya kirafiki dhidi ya Shangani na wakatamka kauli ambazo ni kama wameipuuza kwa kusema: “Yanga wenyewe ndiyo hawa? Watatukoma.” Lakini kejeli hiyo ya Simba imekuja siku moja baada ya Kocha Marcio Maximo kutamka kwamba yupo makini na kila anachofanya na hawezi kuonyesha makucha yake hapa Unguja kwa vile anajua anafuatiliwa. Hivyo licha ya kwamba wanashinda lakini kocha huyo alisisitiza kwamba kinachoonekana sasa ni utangulizi ‘trela’ tu picha lenyewe bado. Vigogo wa Simba walioishuhudia Yanga yenye mastraika wawili Wabrazili ni Makamu wa Rais, Geofrey Nyange ‘Kaburu’, Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili, Kassim Dewji, Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Kamati ya Ufundi, Collins Frisch, Mwenyekiti wa Kamati ya Mashindano Mohamed Nassoro na Makamu wake, Idd Kajuna, wajumbe wengine ni Adam Mgoyi, Mohamed Omary na Hussein Simba. Mbali na hao, kocha wa Simba, Patrick Phiri ambaye pia aliwaona wachezaji wote wa Yanga kwenye mchezo huo akasema Maximo ana kazi ya ziada kurekebisha kikosi chake kwani kina upungufu. “Nimeona mechi lakini bado kuna mapungufu, Maximo anatakiwa kufanya kazi ili kuimarisha kikosi chake,” alisema Phiri huku akiishudia Yanga ikishinda mabao 2-0. “Kazi wanayo, kwa soka lile Maximo anatakiwa kufanya jitihada za makusudi ili kuhakikisha kikosi hakimsumbui msimu ujao, wamecheza chini ya kiwango tofauti na tulivyofikiria,” alisema. Kwa upande wa Dewji yeye alisema: “Kikosi chetu kimecheza vizuri sana (dhidi ya Kilimani City) japokuwa kina udhaifu mdogo ambao kocha atarekebisha, lakini nimeangalia mechi ya Yanga haijanifurahisha, wana kazi. “Kilimani City ni wazuri na wamecheza soka safi ambalo kila mmoja aliyefika kuangalia amefurahia, hata sisi wenyewe tumekubali kuwa timu hiyo ni nzuri ingawa sisi ni wazuri zaidi.” Katika mechi ya Simba ambayo ilikuwa ya kirafiki kama ile ya Yanga na Shangani, Simba ilishinda bao 2-1. Mabao ya Simba yalifungwa na Shaban Kisiga kwa njia ya penalti na jingine lilifungwa na Haruna Chanongo.credit mwanaspoti

 BONYEZA HAPA KUSOMA HABARI NYINGINE 

Emmanuel Okwi sasa akutana na kiboko yake

KAMA Emmanuel Okwi alizoea kudekezwa na viongozi wa Yanga, sasa amekutana na kiboko yake jambo ambalo huenda likamshtua yeye sambamba na wachezaji wengine wa kigeni. Kocha pekee mkuu Mbrazil kwenye Ligi ya Tanzania, Marcio Maximo ametamka kuwa anawajua wachezaji watano tu wa kigeni Yanga na ndio atakaowatumia. Miongoni mwao jina la Okwi ambaye yupo Dar es Salaam halimo. Maximo amesema atafanya kazi na Hamis Kiiza raia wa Uganda, Wanyarwanda Haruna Niyonzima na Mbuyu Twite pamoja Wabrazili Andrey Coutinho na Genilson Santos ‘Jaja’ ndiyo anaowatambua. Pamoja na wachezaji hao watano wanaofanya mazoezi ya pamoja, Yanga ina mkataba na Okwi anayefanya timu kuwa na wachezaji sita wa kigeni idadi ambayo hadi kesho Jumatano siku ya kufunga dirisha la usajili lazima ipunguzwe kwa mmoja kukatwa. Akizungumza na Mwanaspoti, Maximo alisema: “Ninao wachezaji watano tayari wa kutoka nje ya nchi kwenye timu yangu, hao ndiyo nitakaofanya nao kazi msimu huu. “Huyo Okwi sijamwona na hajaripoti kwenye timu yangu nifanyaje? Nitafanya kazi na hao tu.” Awali Kiiza ndiyo alikuwa aachwe, lakini sasa hali imeanza kuwa shwari kwake kutokana na nidhamu yake na jinsi anavyojituma mazoezini. Okwi ambaye alikuwa anapewa kipaumbele lakini alichelewa kujiunga na timu kwa sababu zisizojulikana, inadaiwa kuwa uongozi umemwambia ajieleze kwa barua na baada ya hapo atapewa adhabu ambayo ni siri. Kocha Msaidizi wa Yanga, Leonardo Neiva ambaye pia ni Mbrazili, alisema wamefurahishwa na uwezo wa straika Kiiza na kukiri kuwa ana sababu zote za kubaki Yanga. Aliliambia Mwanaspoti kuwa wamependa vigezo vitatu alivyonavyo straika huyo ambavyo ni nguvu, mipango mizuri ya uwanjani na uwezo wake wa kucheza kwenye nafasi tatu tofauti kwa ufasaha. “Anaweza kucheza kiungo vizuri tu kwani ana nguvu, kasi na vilevile mbinu , ana uwezo mkubwa wa kucheza winga na anatoa krosi nzuri na zenye malengo huku akikimbia kwa kasi, anacheza nafasi ya straika wa mwisho pia,” alisema Neiva.Source mwanaspoti

 >>>>>>>>> BOFYA HAPA <<<<>>>uhungane nasi

Lingine linalosemwa kwenye uhusiano wa Wema Sepetu na Diamond Platnumz.

Ukubwa wa majina yao unawafanya kila inapoitwa leo kuzungumziwa kwenye vyombo mbalimbali vya habari kuhusiana na uhusiano wao wa kimapenzi huku stori nyingi zimekuwa zikitoka zinazowahusu. Wiki chache inasemekana uhusiano huu haukuwa kwenye hali nzuri baada ya mashabiki wa Wema kuanza kampeni ambayo ilikua ikimtaka Diamond Platnumz amrejeshe Wema aliyekua akicheza filamu kama zamani. Mezani kwa Soudy Brown leo ni kuhusu isue hii ambayo kwa sasa inasemekana Diamond na Wema wameachana tena ingawa si mara ya kwanza ila uhakika wa stori tunaungana na Soudy Brown kumsikiliza Wema akizungumzia hili.bonyeza play kusikiliza

>>>>>>>>>> play hapa <<<<<<<<<<<<<<<<<\\\\
Crd millardayo

HUU NDO MSIMAMO WA LIGI KUU YA UINGEREZA (EPL)

TETESI ZA SOKA ZILIZOSHAMILI KWENYE MAGAZETI MBALIMBALI ULAYA YA LEO JUMANNE ZIPO HAPA

Manchester United wamekamilisha majadiliano na Real Madrid na watalipa pauni milioni 63.9 na kuvunja rekodi ya Uingereza kumnunua winga Angel Di Maria (Sky Sports), mchezaji huyo kutoka Argentina huenda akafikia kuuzwa kwa pauni milioni 72, milioni 60 zikilipwa mwanzo na milioni 12 baadaye (Daily Mirror), Juventus wataanza mazungumzo na Arsenal kuhusu Lukas Podolski. Juventus wanamtaka kwa mkopo lakini Arsenal wanataka kumuuza (Daily Telegraph), boss wa Real Madrid Carlo Ancelotti amesema Sami Khedira, 27, hatoondoka licha ya kufuatiliwa na Arsenal, Bayern Munich na Manchester United (Guardian), meneja wa Everton Roberto Martinez amesema bado anaweza kumsajili Samuel Eto'o, 33, au Danny Welbeck, 23, katika wiki ya mwisho ya dirisha la usajili (Times), boss wa Arsenal Arsene Wenger amemuulizia beki mkabaji wa Brazil Luiz Gustavo, 27, anayechezea Wolfsburg (Daily Mirror), Southampton wamepanda dau kwa winga wa Tottenham Andros Townsend, 23, (ESPN FC), meneja wa Southampton Ronald Koeman yuko tayari kuanza kumfuatilia tena winga wa Norwich Nathan Redmond, 20, (Sun), Liverpool watalazimika kuchukua hatua za haraka kumsajili Radamel Falcao, 28, wakati Juventus wakimtaka mshambuliaji huyo wa Monaco kwa mkopo (Daily Star), Fernando Torres hatoondoka Chelsea bila ya mkataba wa kitita cha pauni milioni 8.5 kutolewa. Roma wanamtaka mshambuliaji huyo (Sun), Sunderland wamekuwa na mazungumzo na winga wa zamani wa Chelsea, Salomon Kalou, 29, ambaye pia anatazamwa na Arsenal, Liverpool na Everton (Daily Express), boss wa Sunderland ana matumaini ya kupata jibu iwapo mshambuliaji wa Liverpool Fabio Borini, 23, atajiunga nao au la (Sunderland Echo), West Ham wamemuulizia beki wa Manchester City Micah Richards, 26, ambaye anaonekana huenda akaondoka City wiki hii (Sun), QPR wamehusishwa na kipa wa Reading Alex McCarthy, 24, (Daily Star), AC Milan wanamtaka Samuel Eto'o na Fernando Torres kuziba pengo la Mario Balotelli (Gazetta dello Sport), Juventus wana nafasi kubwa ya kumshawishi Radamel Falcao kujiunga nao kwa mkopo wa mwaka mmoja (Gazetta dello Sport), Lukas Podolski huenda akasaini mkataba wa miaka mitatu na Wolfsburg na watalipa euro milioni 12 kumsajili kutoka Arsenal (L'Equipe). Zimesalia siku saba kabla ya dirisha la usajili kufungwa. Tetesi nyingine kesho tukijaaliwa.credit salim kikeke

BREAKING NEWZ:::PENZI LA WEMA NA DIAMOND TENA BAAAASI WAMEBWAGANA VIBAYA SANA SOMA HAPA

Habari zilizotukia hivi punde ni kwamba wema na diamond wameacahana rasimi leo asubuh,akiongea na kituo kimoja cha redio wema kwa masikitiko akionekana mwenye majonzi alisema please i dont like to talk about it

Stay tune kwa habari zaidi
Source:mzalendohuru.blogspot.com

MASOGANGE AWATUKANA WANAUME MATUSI MAZITO WANAOMPELEKEA HABARI ZAKE KWA JAMAA YAKE WA SAUZI

Kama mnavyojua AGNES MASOGANGE kwasasa yupo BONGO na Yule jamaa yake yupo SAUZI..sasa kutokana na taarifa za kile ambacho MASOGANGE anakifanya hapa mjini kumfikia jamaa yake huko SAUZI kupitia jamaa ambao wanampa ripoti zote kutoka hapa BONGO na hivyo kupelekea kuhatarisha penzi la MASOGANGE na huyo jamaa…MASOGANGE AMEAMUA KUFUNGUKA Kupitia ukurasa wake wa INSTAGRAM aliweka picha hiyo na kuandika kama unavyoona hapa!!!