Wednesday, November 19, 2014

JB kuja na filamu ya soka la Bongo

Muigizaji mahari wa filamu, Jacob Stephan aka JB, amesema yupo mbioni kuandaa filamu kuhusu soka la Tanzania. JB ambaye ni shabiki mkubwa Simba alisema hayo kwenye kipindi cha Kili Chart Show cha EATV baada shabiki mmoja kumuuliza kama ana mpango wa kufanya filamu ya aina hiyo. “Kwa sababu wengi wameguswa nitafanya tena filamu nyingine ya mpira, ambayo nitazungumzia moja kwa moja, mpira wa kitanzania, wazo lako nitalifanyiwa kazi na Jerusalem film,” alisema JB.

0 comments:

Post a Comment