Wednesday, November 19, 2014
|
ENGLAND imewalaza wenyeji Scotland mabao
3-1 katika mchezo wa kirafiki wa kimataifa
usiku huu.
Shukrani kwao, wafungaji wa mabao hayo,
Alex Oxlade-Chamberlain dakika ya 32 na
Wayne Rooney aliyefunga mabao mawili
dakika za 47 na 85, wakati bao pekee la
wenyeji lilifungwa na Andrew Robertson dakika
ya 83.
Kwa kufunga mabao hayo mawili, Rooney
amekuwa mchezaji wa tatu kufunga mabao
mengi katika historia ya timu ya taifa ya
England kutokana na kufikisha mabao 45,
akimpita Jimmy Greaves.
Kikosi cha Scotland kilikuwa: Marshall/Gordon
dk46, Whittaker, R Martin, Hanley/May dk66,
Robertson, Maloney, Mulgrew, Brown/D
Fletcher dk46, Anya/Bannan dk61, C Martin/
Morrison dk46 na Naismith.
England: Forster, Clyne, Cahill/Jagielka dk46,
Smalling, Shaw/Gibbs dk66, Oxlade-
Chamberlain, Milner, Wilshere/Barkley dk87,
Downing/Lallana dk46, Rooney na Welbeck/
Sterling dk46. |
0 comments:
Post a Comment