Thursday, October 02, 2014
|
MSHAMBULIAJI Danny Welbeck amefunga
hat trick yake ya kwanza Arsenal ikishinda
4-1 katika mchezo wa Kundi D Ligi ya
Mabingwa Ulaya usiku huu Uwanja wa
Emirates.
Mshambuliaji huyo aliyenunuliwa kutoka
Manchester United msimu huu, alifunga
mabao hayo katika dakika za 22, 30 na 52
wakati lingine limefungwa na Alexis Sanchez
dakika ya 41- huku bao la wageni likifungwa
na Burak Yilmaz kwa penalti dakika ya 63.
Kipa wa Arsenal, Szcezesny alitolewa kwa
kadi nyekundu dakika ya 60 na bado hiyo
haikuizuia timu ya Arsene Wenger kushinda.
Mchezo mwingine wa Kundi D, Anderlecht
imechapwa 3-0 nyumbani na Borrusia
Dortmund mabao ya Ciro Immobile dakika
ya tatu na Adrian Ramos dakika ya 69 na
79.
Kundi A bao pekee la Ada Turan limetosha
kuipa Atletico Madrid ushindi wa 1-0 dhidi
ya Juventus wakati katika mchezo mwingine
wa kundi hilo, Malmo FF ya Sweden
imeichapa 2-0 Olympiacos ya Ugiriki mabao
yake yakitiwa kimiani na M Rosenberg
dakika ya 42 na 82.
Kundi B, Basel imeichapa 1-0 Liverpool bao
pekee la Marco Streller dakika ya 52, wakati
Real Madrid imeshinda ugenini mabao 2-1
dhidi ya PFC Ludogorets Razgrad.
Wenyeji walitangulia kupata bao dakika ya
sita kupitia kwa Marcelinho kabla ya
Cristiano Ronaldo kufunga kwa penalti mara
mbili dakika ya 11 na 25 kuipa ushindi Real
Madrid.
Katika Kundi C, Zenit St Petersburg imetoka
0-0 na Monaco huku Bayer Leverkusen
ikiitandika 3-1 Benfica, mabao ya Stefan
Kiessling dakika ya 25, Heung-Min Son
dakika ya 34 na Calhanoglu dakika ya 64,
huku Eduardo Salvio akiwafungia Benfica
dakika ya 62. |
0 comments:
Post a Comment