Thursday, October 02, 2014
|
KIUNGO wa Newcastle, Cheick Tiote
amesema kwamba anataka kuondoka klabu
hiyo na amekiri amekuwa katika
mawasiliano na Arsenal.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 28
amedumu kwa miaka minne Tyneside na
kumekuwa na mapendekezo ya kuongezewa
mkataba mpya, lakini sasa mpango huo upo
shakani.
Tiote amewaambia Waandishi wa Habari
nchini kwao kwamba: "Nataka kuondoma.
Nimedumu kwa miaka minne na Newcastle.
Nafikiri nimefikia kikomo ambacho labda ni
wakati mwafaka kutafuta changamoto mpya
sehemu nyingine,"amesema.
Cheick Tiote amesema anataka kuondoka
Newcastle aka sake changamoto mpya na
amekiri juu ya mawasiliano na Arsenal
"NitaeIekeza nguvu zangu katika mechi
zijazo na tune itakuwaje kati ya sasa na
Desemba. Ni kweli kulikuwa kuna
mawasiliano na Arsenal na klabu ya Urusi.
Ningependa kubaki England,". |
0 comments:
Post a Comment