Thursday, October 02, 2014
|
BADO bao moja tu Cristiano Ronaldo afikie
idadi ya mabao ya Raul anayeongoza kwa
kufunga zaidi kwenye Ligi ya Mabingwa
Ulaya.
Ronaldo usiku huu amezidi 'kuisuuza roho'
ya kocha wake, Carlo Ancelotti baada ya
kufunga mabao mawili katika ushindi wa
2-1 ugenini dhidi ya PFC Ludogorets
Razgrad.
Wenyeji walitangulia kupata bao dakika ya
sita kupitia kwa Marcelinho kabla ya
Cristiano Ronaldo kufunga kwa penalti mara
mbili dakika ya 11 na 25 kuipa ushindi Real
Madrid.
Mfalme wa mabao; Nyota wa Real Madrid,
Cristiano Ronaldo amebakiza bao moja
kufikia rekodi ya Raul katika Ligi ya
Mabingwa Ulaya
Mwanasoka huyo bora wa dunia
sasa anatomize mabao 70 aliyofunga katika
Ligi ya Mabingwa Ulaya, moja nyuma ya
Raul aliyefunga mara 71.
Anafunga mabao hayo siku moja baada ya
kocha Ancelotti kukaririwa akisema "Ni
mchezaji bora zaidi niliyewahi
kumfundisha,".
Kipenzi huyo wa mashabiki wa Manchester
United sasa anamzidi kwa mabao mawili,
mpinzani wake Lionel Messi wa Barcelona,
ambaye ana mabao 68. Ruud van Nisterlooy
anashika nafasi ya nne kwa mabao yake 56,
Thierry Henry mwenye mabao 50 ni wa tano,
Alfred de Stefano mwenye mabao 49 ni wa
sita, Andriy Shevchenko mwenye mabao 48
ni wa saba, wakati Eusebio mwenye mabao
46 sawa na Filippo Inzaghi wanashika nafasi
ya nane. Didier Drogba anakamilisha orodha
ya wachezaji 10 waliofunga mabao mengi
Ligi ya Mabingwa kwa mabao yake 42. |
0 comments:
Post a Comment