Friday, October 10, 2014

SIMBA SC KUKIPIGA NA TIMU HII KUBWA YA SOUTH AFRICA KUJIANDAA DHIDI YA YANGA

Katika kujiandaa na mchezo dhidi ya Yanga tarehe 18 Oktoba 2014, Simba itacheza mechi ya kujiandaa kwa kuingia kwenye uwanja na club kubwa ya Afrika Kusini. Simba ambayo iliondoka nchini jana keshokutwa (Jumamosi) itacheza mchezo wa kirafiki na Orlando Pirates mjini Johannesburg, Afrika Kusini. Katika mchezo huo, Simba SC itawakosa wachezaji wake walio timu ya taifa ya Tanzania, Taifa Stars na Uganda, The Cranes- ambao wanatarajiwa kujiunga na wenzao kuanzia Jumatatu. Hata hivyo, mshambuliaji Mganda, Emmanuel Okwi aliyekwenda kujiunga na The Cranes yeye hatakwenda kabisa Afrika Kusini, kwa sababu timu yake hiyo ya taifa itakuwa na mechi ya kufuzu AFCON katikati ya wiki. Wachezaji wa Simba SC walioko Stars ni; Miraji Adam, Joram, Mgeveke,Jonas Mkude, Amri Kiemba, Said Ndemla na Haruna Chanongo ambao wote watakwenda Afrika Kusini Jumatatu. Simba SC imefikia katika hoteli ya Eden Vale Petra na itakuwa inafanya mazoezi kwenye viwanja wa Eden Vale mjini Johannesburg.

KAMA BADO UJAJIUNGA NASI ILI KILA TUKIPATA HABARI ZIKUFIKIE KIRAHISI KWENYE FACEBOOK YAKO BOFYA HAPA 

0 comments:

Post a Comment