 |
| Msanii wa filamu nchini Irene Uwoya amesema
anajiandaa kuachia filamu yake mpya iitwayo
‘Kisoda’.
Uwoya amesema alisafiri hadi Afrika Kusini ili
kutafuta location tofauti zitakazoifanya filamu
hiyo kuvutia.
“Filamu ya Kigoda ni filamu ya aina yake katika
filamu ambazo nimewahi kuzifanya,” ameiambia
Bongo5. “Filamu inahusu drama and music,
imeshagharimu pesa nyingi sana. Ndani utaona
watu wakicheza muziki na maisha ya wasanii.
Kwahiyo itakuwa tayari hivi karibuni na
tutatangaza ikiwa tayar kwenda sokon.”
Katika hatua nyingine, Uwoya amekanusha uvumi
kuwa ana uhusiano na msanii wa Soundtrack,
Msami ambaye anadai ameshiriki kwenye filamu
hiyo.
“Msami sijawai kuwa na mahusiano naye, alikuwa
kama msanii mwenzangu. Hata ule ukaribu wake
na mimi ambao ulizua tetesi za kuwa na
mahusiano naye ni kutokana na hii filamu.
Kwahiyo watu wajue ilikuwa ni kazi tu.” CRD BONGO5 |
KAMA BADO UJAJIUNGA NASI ILI KILA TUKIPATA HABARI ZIKUFIKIE KIRAHISI KWENYE FACEBOOK YAKO BOFYA HAPA
0 comments:
Post a Comment