Thursday, October 09, 2014

MASKINI KIJANA HUYU, ANUSURIKA KUUAWA KWA KUCHOMWA MOTO AKIDHANIWA NI MWIZI!

MTU mmoja aliyefahamika kwa jina la Richard Osward (40) mkazi wa Tabata Segerea, hivi karibuni alinusurika kuuawa kwa kuchomwa moto na wananchi baada ya kuhisiwa kuwa mwizi alipokutwa alfajiri akiwa na mfuko ambao ndani yake kulikuwa na bomba, huko Segerea. Richard Osward aliyechomwa moto na watu wenye hasira kali akidhaniwa kuwa ni mwizi. Akizungumza kwa shida akiwa katika wodi namba 23 iliyomo ndani ya Jengo la Sewa Haji katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili, Richard alisema tukio hilo lilimkuta akiwa ameongozana na rafiki yake aliyemtaja kwa jina la Moses na kwamba walikuwa wakielekea Gerezani, Kariakoo ambako wanajishughulisha na ufundi wa magari.

0 comments:

Post a Comment