Saturday, October 04, 2014
|
Ni sheeedah! Msanii wa Bongo Fleva, Nasibu
Abdul ‘Diamond’ amecharukia gari aina ya
BMW 545 alilozawadiwa mwandani wake,
Beautiful Onyinye wa Bongo, Wema Isaac
Sepetu ‘Madam’ ambaye ni Miss Tanzania
2006/07, akipinga gari hilo kupewa na meneja
wake, Martin Kadinda.
Gari aina ya BMW 545i alilozawadiwa Wema
Isaac Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ na meneja
wake, Martin Kadinda.
DIAMOND ACHANGANYIKIWA
Habari za kipekepeke zilidai kuwa, taarifa ya
Kadinda kumpa zawadi ya gari Wema kwenye
pati ya bethidei yake Jumapili iliyopita,
nyumbani kwake, Kijitonyama, Dar
zilimchanganya Diamond na kudai kwamba ni
kitu ambacho hakiwezekani kwa maana
anamfahamu vyema Kadinda kuwa hana
uwezo huo wa kununua BMW la zaidi Sh.
milioni 56 za madafu. |
|
Wema Sepetu ‘Beautiful Onyinye’ akifungua
shampeni katika bethidei yake.
Chanzo hicho kiliweka wazi kwamba mkali
huyo anayekimbiza na Ngoma ya
Mdogomdogo alihamaki baada ya kupata
taarifa kuwa siyo yeye peke yake aliyekabidhi
zawadi ya gari (Nissan Murano) kwa maana
aliamini mwenye zawadi ya gari alikuwa ni
yeye tu ambayo ilikuwa ‘surprise’ kwa
mpenzi wake huyo. |
|
Wema Sepetu ‘Beautiful Onyinye’akipokea
funguo ya gari la zawadi kutoka kwa Meneja
wake.
BOFYA HAPA KUPATA ‘UBUYU’
“Unaambiwa Diamond kachanganyikiwa
kabisa kusikia Wema kapewa gari, tena BMW
na mbaya zaidi aliyempa gari ni Kadinda
huku yeye akiamini kabisa zawadi aliyotoa
kwa mpenzi wake asingeweza kupata kwa
mtu mwingine yeyote, mwenyewe anasema
amedhalilishwa kwani hawezi kutoa gari
kisha mwanaume mwenzake naye atoe gari,”
kilidai chanzo hicho. |
|
Mpashaji huyo alizidi kufafanua kwamba
baada ya kupokea taarifa hizo na kuona
kwenye vyombo vya habari na mitandao
mbalimbali akiwa nje ya nchi, Diamond
alianza kufanya utaratibu wa kurudi nchini
akitokea Canada ili kujua vizuri kuhusu
undani wa hilo gari.
“Yaani ninyi mtasikia, nakwambia kimenuka
maana Diamond aliposikia na kusoma habari
za BMW la Wema alianza kufanya utaratibu
wa kurudi Bongo ili kupata ufafanuzi zaidi,”
kilisema chanzo hicho. |
|
Kwa upande wake Kadinda ameendelea
kusisitiza kwamba yeye ndiye aliyenunua gari
hilo na kumkabidhi Wema ikiwa ni michango
ya watu wanaomsapoti mwanadada huyo.
Kuhusu gari hilo, watu kibao wamekuwa
wakitajwa kulinunua akiwemo
mfanyabiashara Mkongo mwenye jina
linaloanza na herufi S na mume wa mtu
ambaye ni kigogo wa Mamlaka ya Mapato
Tanzania (TRA) jijini Dar anayetajwa kwa
herufi moja ya L.
WEMA VIPI?
Jitihada za kumsikia Wema ziligonga
mwamba baada ya simu yake kuita bila
kupokelewa na hata alipofuatwa nyumbani
kwake hakuwepo hivyo juhudi za kupata lake
la moyoni zinaendelea. Stay tuned kwani
inavyoonekana nyuma ya pazia ya gari hilo
kuna siri kubwa! |
Gpl
0 comments:
Post a Comment