Wednesday, October 08, 2014

ARSENE WENGER AMPA MOURINHO DONGO LINGINE ZITO KUHUSIANA NA DIEGO COSTA

KOCHA Arsene Wenger ameshtukia ujanja wa mpinzani wake Jose Mourinho juu ya majeruhi ya straika Diego Costa. Wenger anayeinoa Arsenal, ambayo Jumapili iliyopita ilimenyana na kikosi cha Chelsea alisema anahisi Mourinho anawachezea akili wapinzani wake kuhusu madai ya majeruhi ya misuli ya straika wake huyo. Alipoulizwa kuhusu maoni yake juu ya straika huyo ambaye ni kinara wa mabao kwenye Ligi Kuu England mpaka sasa msimu huu, Wenger alitabasamu kisha akasema: “Kusema kweli, unapomtazama fowadi huyo uwanjani haonekani kuwa ni majeruhi. “Amekuwa na tatizo la misuli kwa muda mrefu na tuliliona hilo kwenye fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita, lakini nilipomtazama kwa siku za karibuni, ni ngumu kuamini ni aina gani ya majeruhi ya misuli yanayomsumbua.”

0 comments:

Post a Comment