Sunday, September 21, 2014
|
Wiki moja baada ya kuifunga klabu bingwa ya
Tanzania Bara Azam FC kwa magoli 3-0
kwenye mchezo wa ngao ya hisani, leo hii
watoto wa Jangwani Dar Young Africans
wamekutana na kisanga kizito kutoka kwa
Mtibwa Sugar.
Katika mchezo huo uliopigwa kwenye dimba la
Manungu mjini Morogoro umeisha kwa Yanga
kutandikwa 2-0 na vijana wa Mecky Mexime.
Magoli ya Mtibwa yalifungwa na Mussa
Hassan Mgosi katika dakika 15, kabla ya Ame
Ally kuandika goli la pili dakika ya 82 ya
mchezo huo.
Katika mchezo huo wa leo shujaa wa Yanga
katika mechi dhidi ya Azam FC mbrazil Jaja
alikosa penati.
Matokeo mengine kwenye ligi hiyo ni kama
ifuatavyo: Stand 1-4 Ndanda, Azam 3-1 Polisi
Moro, Prisons 2-0 Ruvu Shooting, Mgambo 1-0
Kagera, Mbeya City 0-0 JKT Ruvu |
0 comments:
Post a Comment