Friday, September 19, 2014
|
Marais wengi Afrika wamemtembea Joshua
wakitafuta kuombewa
Kanisa lililoporomoka mjini Lagos wiki
jana , na kuwaua watu wengi, lilikuwa
linamilikiwa na mhubiri anayesifika sana
nchini Nigeria, TB Joshua.
Tomi Oladipo anatufichulia haiba ya
mhubiri huyu ambaye anadai amewaponya
watu wakiwemo vipofu na waathiriwa wa
HIV.
TB Joshua anadai kuwahi kutabiri matukio
mengi kuanzia kwa kifo cha aliyekuwa
gwiji wa muziki, Michael Jackson, hadi
kupotea kwa ndege ya Malaysia ya MH370"
Anajiita mtume na ni mmoja wa wahubiri
mashuhuri sana nchini Nigeria ambako
makanisa kama lake ni mengi kupindukia.
Alizaliwa mwaka 1963 tarehe 12 Juni katika
familia maskini, akidai kwamba alikaa
kwenye tumbo la mamake kwa miezi 15.
Baadaye katika maisha yake, anadai kuona
kwenye ndoto yake manabii wakimtaka
kuhubiri na kufanya miujiza. |
0 comments:
Post a Comment