Thursday, September 04, 2014
 |
Pamoja na kwamba mapromoter Wanigeria
walioandaa show ya Diamond iliyoshindwa
kufanyika weekend iliyopita mjini Stuttgart,
Ujerumani baada ya kutokea vurugu kubwa,
upande wa Diamond Platnumz amesema kwake
haoni kama tukio hilo limemchafua kwa namna
yoyote na badala yake anaona limempa ‘kiki’.
“Sidhani kwasababu karibuni asilimia tisini
walijua nini kinachoendelea hawakujua kabisa
tatizo lilikuwa kwa msanii…hiki kitu kiko wazi
na hata promota nasikia amezungumza
kuwaambia kwamba halikuwa tatizo la msanii”
amesema Diamond kupitia 255 ya Clouds Fm.
Diamond amesema kuwa baada ya tukio hilo
asubuhi yake vyombo vingi vya habari vya
Ujerumani viliandika habari hiyo ambayo kwa
upande wake hiyo ni faida.
“mi nachokiona sana sana naona busta tu
kwasababu asubuhi yake iliandikwa katika blog
kibao za Ujerumani magazeti ya Ujerumani,
katika vitu viiingi vya Ujerumani viliandika
kama ilitokea hivi na hivi na hivi afu kila
ikiandikwa itamuandika Diamond wanaweka
picha ya Diamond. So kwa namna moja ama
nyingine Mwenyezi Mungu alitumia njia ile
kufanya watu wa Ujerumani kama kuna mtu
anaitwa Diamond wajue kuna mtu anaitwa
Diamond”.
Hata hivyo kwa upande mwingine Platnumz
amesema alijisikia vibaya pamoja na kwamba
alilipwa pesa yote lakini kama msanii kuna kitu
muhimu alichokikosa.
“Kiukweli nilijiskia vibaya kwasababu msanii
hakuna kitu unachokifurahia kwanza kama
show ijae kwasababu show ikijaa kwanza ni
credit, ni cv kubwa sana unajua unavyopost ile
picha umejaza unawatengenezea promoters
wengine kuona kama huyu mtu anakubalika”. |
 |
Uharibifu uliotokana na vurugu hizo |
KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BOFYA HAPA ILI KILA NIKIPATA HABARI ZIKUFIKIE KIRAHISI PUNDE NIZIPATAPO
Posted via Blogaway
0 comments:
Post a Comment