Monday, August 25, 2014

SIMBA SC YAIJIBU YANGA SC, YAUA 2-1 AMAAN USIKU HUU

Mohamed Abdallah, Zanaibar Kikosi cha Simba kinachoongozwa na Patrick Phiri, kimeishinda Kilimani ya daraja la pili Zanzibar kwa mabo 2-1 katika mechi ya kirafiki iliyopigwa kwenye Uwanja wa Amaan mjini hapa. Ingawa ina kikosi kinachoundwa na Kilimani wengi kweli, Chipukizi ilionyesha soka safi na la kuvutia. Timu hiyo inasifika kwa soka la kasi na pasi nyingi ikiwa Simba wakati mgumu kwa muda mwingi. Simba ndiyo ilianza kupata bao kupitia Amissi Tambwe kwa mkwaju wa penalti lakini Kilimani wakasawazisha katika dakika ya 78. Simba walifanikiwa kupata bao la pili katika dakika ya 84 kupitia Haruna Chanongo.NA MDADISI BLOG /FESTOSAIMON

0 comments:

Post a Comment