Real Madrid
imekubali kumuachia
Angelo Di Maria
ambaye anatua Man
United kw akitita
cha pauni milioni
64.
Uhamisho wake
utavunja rekodi na
kuwa ghali zaidi
England ukiupita ule
wa pauni milioni 50
wakati Fernando
Torred alipotua
Chelsea akitokea
Liverpool.
Di Maria raia wa
Argentina,
anatarajia kutua
jijini Manchester
leo kwa ajili ya
vipimo na kumalizana
na wenyeji wake.
Kocha Carlo
Ancelotti wa Madrid
amethibitisha kwamba
mkali huyo alikwenda
kuwaaga mazoezini
kwamba anaondoka.
Man United imekuwa
ikifanya juhudi
kujiimarisha baada
ya kusuasua kwa
msimu mzima na pia
kuanza vibaya msimu
mpya kwa kipigo na
sare dhidi ya
Swansea na
Sunderland. NA MDADISIBLOG/FESTOSAIMON |
0 comments:
Post a Comment