Mohamed Abdallah,
Zanzibar
Andrey Coutinho
amefanikiwa kupiga
bao na kuisaidia
Yanga kuifunga
Shangani
inayoshiriki Ligi
Daraja la Pili hapa.
Yanga imefanikiwa
kuibuka na ushindi
wa mabao 2-0, moja
likiwa
limesababishwa na
Salum Telela ambaye
alipiga krosi safi
mabeki wa Shangani
wakajifunga.
Mechi hiyo kwenye
Uwanja wa Amaan
mjini hapa, ilikuwa
nzuri nay a kuvutia.
Coutinho alionekana
kuwa fiti zaidi huku
Mbrazili mwenzake,
Jaja akibanwa.
Yanga ilicheza kwa
kuelewana tokea
mwanzo, lakini
baadaye Shangani nao
walijibu
mashambulizi na
kuifanya mechi kuwa
ya ushindani.
Chini ya Marcio
Maximo, Yanga
itacheza mechi
nyingine moja ya
kirafiki Jumatano
kabla ya kurejea
jijini Dar. |
0 comments:
Post a Comment