Wednesday, August 27, 2014

Official: Everton yamsaini Samuel Eto’o – aizungumzia Liverpool

Mshambuliaji wa zamani wa klabu ya FC Barcelona na Chelsea Samuel Eto’o amekamilisha usajili wa kujiunga na Klabu ya Everton. Eto’o ambaye alikuwa akikaribia kujiunga na liverpool amejiunga na Everton na kusaini mkataba wa kuitumikia klabu hiyo kwa miaka miwili. Nahodha huyo wa timu ya taifa ya Cameroon ameripotiwa kusononeshwa na uhamisho wake kwenda Liverpool kufeli wakati akiwa tayari ameshafanya mpka vipimo vya afya. Eto’o anatarajiwa kuanza kuichezea Everton wikiendi hii kwa mchezo dhidi ya Chelsea ambayo aliitumikia msimu uliopita.

 KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BOFYA HAPA ILI UPATE HABARI ZA KIMICHEZO KIRAHISI ZAID 

0 comments:

Post a Comment