Saturday, August 30, 2014
|
Mabingwa wa England,
Manchester City wameanza
kuonja joto ya jiwe wa Ligi
Kuu England baada ya leo
kulala kwa bao 1-0.
Stoke City ambao
waliinyanyasa Man City
msimu uliopita, leo
‘wameifanyia mbaya’ kwa
kuichapa kwa bao 1-0 tu.
Mame Diouf ndiye alikuwa
shujaa wa Stoke City
waliokuwa nyumbani baada ya
kuwapangua viungo na mabeki
wa wageni wao kabla ya
kupachika bao akipiga mpira
uliompita kipa Joe Hart
katikati ya miguu yake,
unaweza kusema topo.
Juhudi za Man City kutaka
kuchomoa 'kashfa' hiyo
ziligonga mwamba. |
Posted via Blogaway
0 comments:
Post a Comment