Saturday, August 30, 2014

FERGUSON LEO AMEUDHIKA MNO MAN UNITED MECHI YA TATU HAKUNA USHINDI

Maudhi matupu: Kocha wa zamani wa Manchester United, Sir Alex Ferguson (mbeke) akiwa na David Gill na Sir Bobby Charlton wakitazama mchezo wa timu hiyo leo ikilazimishwa sare ya 0-0 na Burnley. United imekuwa ikisuasua tangu kustaafu kwa Ferguson mwaka jana. Makocha wawili wamekwishapewa timu, David Moyes aliyetimuliwa mwishoni mwa msimu uliopita na Ryan Giggs akakaimu kumalizia msimu, kabla ya msimu huu kuajiriwa Louis Van Gaal ambaye leo amefikisha mechi ya tatu bila ushindi, sare mbili ugenini, nyingine 1-1 na Sunderland na kufungwa moja nyumbani na Swansea City 2-1.

Posted via Blogaway

0 comments:

Post a Comment