Saturday, August 30, 2014

Baada ya kuondoka kwa Torres – huyu ndio mshambuliaji mpya aliyesajiliwa na Chelsea

Usiku wa jana mshambuliaji wa kimataifa wa Spain Fernando Torres alikamilisha usajili wake wa mkopo wa miaka miwili kutoka Chelsea kwenda AC Milan. Huku yakiwa hajapita hata masaa 24 tangu Torres aondoke, Jose Mourinho amekamilisha usajili wa mbadala wa Torres, mshambuliaji wa kimataifa wa Ufaransa Loic Remy. Remy ambaye alifeli vipimo vya afya alipokuwa akikaribia kujiunga na Liverpool mwanzoni mwa dirisha la usajili, amejiunga na Chelsea kwa ada ya uhamisho wa paundi millioni 10 kutoka QPR. Remy anachukua nafasi ya Torres na kuungana na Didier Drogba katika kumsaidia Diego Costa. Wakati huo huo Alex Song amejiunga na West Ham kwa mkopo kutoka FC Barcelona.

Posted via Blogaway


Posted via Blogaway

0 comments:

Post a Comment