Sunday, August 24, 2014

Fifa yataka kina Ronaldo wakacheze Morocco (kwenye EBOLA)

SHIRIKISHO la Soka la Kimataifa (Fifa) limethibitisha kwamba Morocco itakuwa mwenyeji wa michuano ya Klabu Bingwa Dunia kwa mwaka wa pili mfululizo licha ya kuwapo na wasiwasi wa ugonjwa wa Ebola. Maeneo ya Afrika Magharibi yamekuwa tishio kubwa kutokana na kuibuka kwa virusi hivyo vya ugonjwa wa Ebola na kuibua wasiwasi kama ni mwafaka kwa michuano hiyo kufanyika Morocco Desemba mwaka huu. Hata hivyo, Fifa imetangaza kwamba hakuna haja ya kuwa na wasiwasi na timu zitakuwa kwenye mazingira mazuri. “Afya za wachezaji, maofisa na mashabiki ni kitu kinachozingatiwa zaidi na Fifa kwenye michuano yake,” ilibainisha taarifa ya shirikisho hilo. “Kwa mujibu wa taarifa zilizopo ni kwamba hakuna kesi yoyote ya Ebola iliyoripotiwa Morocco, hivyo hakuna sababu ya kuzungumzia kubadili sehemu ya kufanyika kwa michuano hiyo. Kama kutakuwa na mabadiliko tutatoa taarifa.” Miongoni mwa timu zitakazoshiriki ni Real Madrid inayochezewa na masupastaa wa dunia, Cristiano Ronaldo, Gareth Bale, James Rodriguez na Toni Kroos.

0 comments:

Post a Comment