Saturday, August 30, 2014
|
Mechi ya mwisho ya Premier League leo hii
ilikuwa kati ya vijana wa Jose Mourinho
Chelsea dhidi ya vijana wa Roberto Martinez
Everton.
Mchezo huo wa kuvutia uliopigwa kwenye
dimba la Goodson Park umeisha kwa Chelsea
kupata ushindi mzito na mkubwa kuliko
wowote kwenye premier league msimu huu.
Magoli ya mapema ya Diego Costa na Ivanovic
yaliwaweka Chelsea mbele kwa 2-1 mpaka
timu zilipoenda mapumziko – Kevin Mirallas
aliifungia Everton goli la kwanza dakika chache
kabla ya kipindi cha kwanza kuisha.
Kipindi cha pili Everton walirudi kwa kasi
wakijaribu kusawazisha lakini kwenyw dakika
ya 67, Coleman akajifunga na kuiongezea
Chelsea uongozi, lakini Naismith akapunguza
pengo dakika 2 baadae, kabla ya Nemanja
Matic kuongeza goli la 4 kwa Chelsea.
Samuel Eto’o akicheza mechi yake ya kwanza
akiwa na Everton akafunga bao la 3 dk 76,
lakini dakika 2 baadae Ramirez akapiga
mkwaju wa 5 na Diego Costa kwa mara
nyingine tena akafunga mahesabu kwa Chelsea
kwa kufunga goli la 6 kwenye dakika 90.
Hadi mwisho wa mchezo matokeo yalikuwa
yakisomeka 6-3. |
0 comments:
Post a Comment