Sunday, August 24, 2014

DI MARIA SASA NI MOJA, MBILI, TATU, NNE.....

Muda wa mshambuliaji Angelo Di Maria kuondoa Real Madrid unaanza kuhesabika. Pamoja na kutangaza dau jipya la zaidi ya pauni milioni 70 ili Manchester United impate, lakini inaonekana Madrid imeshindwa kumzuia. Kwani leo asubuhi hakuonekana mazoezini na kitendo cha kocha Carlo Ancelotti kutomjumuisha kwenye mechi za Super Cup ya Hispania, inaonyesha kiasi gani hayuko kwenye hesabu za timu hiyo. Siku nne zilizopita, Cristiano Ronaldo na Sergio Ramos walizungumza na uongozi na kuutaka ufanye juhudi kumbakiza. Lakini Muargentina huyo anaonekana kuchoshwa na kutopewa heshima yake, hivyo anaweza kuondoka ndani ya leo au kesho. Na mdadisiblog/festosaimon

0 comments:

Post a Comment