Monday, August 18, 2014
MAN CITY YAANZA NA MOTO WAKE LIGI KUU ENGLAND
MABINGWA watetezi wa Ligi Kuu ya England, Manchester City wameanza vizuri harakati za kutetea taji lao, kufuatia ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Newcastle United, Uwanja wa St. James Park.
Katika mchezo huo uliotanguliwa na maombelezo ya Liam Sweeney na John Alder, waliofariki kwenye ajali ya ndege ya MH17, City ilipata bao moja kila kipindi. Alianza kiungo David Silva dakika ya 39, kabla ya mshambuliaji Sergio ‘Kun’ Aguero kupiga la kuhakikisha ushindi dakika ya 90- siku chache baada ya nyota hao wote kusaini mikataba mipya na timu hiyo ya Etihad.
Kikosi cha Manchester City kilikuwa; Hart, Clichy, Kompany, Dimichelis, Kolarov, Toure, Fernando, Nasri/Milner dk77, Jovetic/ Fernandinho dk72, Silva na Dzeko/Aguero dk81. Newcastle United; Krul, Janmaat, Williamson, Coloccini, Dummett, Anita/Obertan dk62, Gouffran/Aarons dk73, Colback, Sissoko, Cabella na Riviere/Perez dk80.
Na mdadidiblog/festo saimon
BONYEZA HAPA KUHUNGANA NA BLOG HII ILI UPATE HABARI MBALIMBALI PUNDE ZINAPOTUFIKIA
Sunday, August 17, 2014
LIVERPOOL YAANZA VYEMA LIGI KUU ENGLAND, WATAKATIFU WAKALIA 2-1 SWAAFI ANFIELD...MAMBO YA STERLING NA STURRID
Shukrani kwake, mshambuliaji wa kimataifa wa England, Daniel Sturridge aliyefunga bao la ushindi dakika ya 79 na kumpa mwanzo mzuri Brenden Rodgers aliyeukosakosa kidogo ubingwa msimu uliopita akizidiwa kete na Manchester City.

Sterling alitangulia kuwafungia Wekundu hao dakika ya 23, kabla ya Nathaniel Clyne kuwasawazishia Watakatifu dakika ya 56.
Kikosi cha Liverpool kilikuwa; Mignolet, Manquillo, Skrtel, Lovren, Johnson, Henderson, Gerrard, Lucas/Allen dk63, Sterling, Coutinho/Lambert dk76 na Sturridge.
Southampton: Forster, Clyne, Fonte, Yoshida, Bertrand, Wanyama, Schneiderlin, Tadic/Long dk73, Ward-Prowse, S Davis/Isgrove dk82 na Pelle.
Katiba Mpya hakieleweki

Dar es Salaam. Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG), Jaji Frederick Werema amesema mchakato wa Katiba Mpya ukikwama kufika mwisho kutokana na mvutano unaoendelea wa makundi mawili kushikilia misimamo yao, kutafanyika marekebisho ya 15 katika Katiba ya sasa ya mwaka 1977 ili kuruhusu kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu mwaka 2015.
Pia, ameipongeza iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba kwa kazi nzuri waliyoifanya kwa kuandaa Rasimu bora na kuwaomba wajumbe wake kuwa na ngozi ngumu ya uvumilivu katika kipindi hiki na waepuke kurushiana maneno na watu wanaowakejeli.
Jaji Werema aliyasema hayo jana wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam kuelezea mchakato huo ulipotoka, ulipofika na unakokwenda huku akitumia Sheria ya Mabadiliko ya Katiba na Rasimu ya Katiba kufafanua baadhi ya mambo.
Mwanasheria huyo, akijibu swali aliloulizwa kuwa Bunge Maalumu la Katiba linaendelea wakati wajumbe kutoka Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) wakiwa hawashiriki, Je, ikishindikana kupatikana kwa theluthi mbili itakuaje? Alisema: “Katika kamati theluthi mbili inatosha, lakini kule mwisho (katika kura ya maoni ya kuipitisha Katiba itakayopendekezwa) kama tutafika darajani, hilo ni suala la siku za usoni.
“Kama tutafika huko na kukuta hakuna pa kutokea, tutarudi bungeni (Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania) na kufanya marekebisho ya 15 katika Katiba ya sasa ya mwaka 1977 kama uwepo wa Tume huru ya Uchaguzi, mgombea binafsi na kupunguzwa kwa mamlaka ya Rais, vitu ambavyo vimekuwa vikizungumzwa sana na wananchi,” alisema Jaji Werema.
Kuhusu madaraka ya Rais kulivunja au kulisitisha Bunge hilo, Jaji Werema alisema “Sheria haimruhusu Rais kulivunja au kulisitisha na katika maongezi yangu na yeye (Rais Kikwete) nilimweleza kwamba hana madaraka hayo.”
Aliongeza: “Nimemwambia hana mamlaka ya kusimamisha, hana mamlaka ya kulivunja na wala asifikirie kwani Sheria haikumpa mamlaka na akifanya hivyo atakuwa anavunja Katiba.”
Jaji Werema alisema mamlaka ya Bunge hilo inatokana na Sheria ya Mabadiliko ya Katiba inayolitaka kujadili na kupitisha Rasimu iliyopendekezwa na Tume kisha kuandaa Katiba na kuipeleka kwa wananchi kwa ajili ya kupigiwa kura ya maoni.
“Kisheria maana ya kujadili ni kuboresha, kubadilisha na kuweka jambo vizuri na hii siyo mimi bali tulikubaliana wote na kanuni zikaandaliwa,” alisema Jaji Werema.
Kuhusu mabadiliko ya kanuni ilizozifanya Bunge hilo wakati Ukawa wakiwa hawapo alisema: “Tulifanya hivyo kwani Rais (Kikwete) amesema siku 60 alizoongeza zikiisha hawezi kuongeza tena, hivyo tumefanya hivyo ili kuwezesha siku hizo zitoshe.”
Aprili 16 mwaka huu, wajumbe wa Ukawa kutoka vyama vya Chadema, CUF, NCCR-Mageuzi na baadhi ya wajumbe kutoka kundi la 201 walisusia kushiriki shughuli zote za Bunge hilo hadi pale Rasimu iliyowasilishwa na Jaji Warioba iheshimiwe kutokana na kubeba maoni na mapendekezo ya wananchi.
Hata hivyo, Bunge hilo liliendelea na vikao vyake hadi lilipoahirishwa Aprili mwaka huu kupisha Bunge la Bajeti na Agosti 5 mwaka huu. Lilirejea tena na kuanza vikao vyake huku wajumbe wa Ukawa wakiwa wameendelea kushikilia msimamo wao.
Credit mwananchi
Hatimaye Masanja aamua kufungikia ishu ya Diamond na Wema kwa kuwapa ushauri 'mzito'
Baada ya uhusiano wa diamond na wema kuingia katika misukosuko na diamond kutoa ujumbe mzito kumhusu wema sepetu, mchekeshaj maarufu hapa bongo masanja mkandami ameamua kufua ya moyoni kuhusiana na uhusiano wa wawili hawa.
masanja alisema haya “Street pastor anasema.. hili swala la diamond na wema nadhani mungu amemuhurumia mmoja wapo kati ya hao wawili.
kama wangekuwa watu wa kuoana wangesha oana uchumba gani mrefu kama wanasomea udokta???? rafiki yangu nasib, kama kweli mlipendana kwa dhati hizo kasoro zinarekebishika, maana hakuna mwanadamu aliye sahihi kwan hata ww nasib unamapungufu yako. na wewe dada yangu wema lazima ujue mme ndio kichwa cha nyumba kwa maelezo hayo inaonyesha haumsikilizagi mwenzio omba msamaha tenaaa na tena na ukubali kubadilika.
mi sipendi mkiwa mnaongozana wote kwenye ma show ya usiku mme kafanye kazi mke abaki home ukirudi mwili umepoa hata ujauzito unaingiaa!! sasa woote stejini mkirudi miili ya moto si mtazaa popompoo jamaniii!! nitafurahi kusikia tofauti zenu mmezimaliza kwa amani ili mashabiki wenu wasijisikie vibaya.” Alimaliza masanja.!
BOFYA HAPA KUHUNGANA NA BLOG HII ILI UPATE HABARI KIRAHISI PUNDE ZITUFIKIAPO
PERUZI KURASA ZA MBELE NA NYUMA ZA MAGAZETI MBALIMBALI YA LEO JUMAPILI
VAN GAAL ASEMA KIPIGO CHA JANA KITAPOTEZA KUJIAMINI MAN UNITED, AKIRI PIA IPO HAJA YA KUSAJILI, HASWA MABEKI
Bao la Gylfi Sigurdsson dakika ya 72 lilimvuruga kocha mpya wa United, Van Gaal kuftia ushindi mfululizo katika mechi sita za kujiandaa na msimu, Mashetani hao Wekundu wakifungwa kwa mara ya kwanza nyumbani katika mchezo wa ufunguzi ndani ya miaka 42.
"Unaposhinda kila kitu katika wakati wa maandalizi na kuja kufungwa mechi ya kwanza, hiyo haiwezi kuwa mbaya," amesema. "Tumejijengea hali ya kujiamini kwa kiasi kikubwa na kisha itaondoka kwa sababu ya matokeo haya,".’

Mholanzi huyo alilazimika kuwachezesha kwa mara ya kwanza katika Ligi Kuu ya England Jesse Lingard na Tyler Blackett, akiwa amesaini wachezaji wawili tu wapya— Ander Herrera na Luke Shaw msimu huu.
Alipoulizwa kama kipigo hicho kitamlazimu kuingie sokoni kusajili kuboresha kikosi, Van Gaal alisema: "Nilifikiri hivyo mkabla ya mechi hii, hivyo hakuna tofauti. Wakati tunacheza Marekani niliona kama hivyo. Kweli tunahitaji mabeki. Lakini huwezi kusema hivyo, kwa sababu tumepoteza mechi moja na tumeshinda nyingine zote, hiyo ni beki. Ni timu ambavyo tumecheza,".
Katika staili yake maarufu, Van Gaal, Mholanzi hiyo hakumnyooshea kidole yeyote baada ya mechi. Kocha huyo mpya wa United, aliwalaumu wachezaji wake kwa kucheza ovyo. Pia alisema walikosa hali ya kujiamini na hawakucheza kitimu.
"Ni siku mbaya sana kwetu. Imewaangusha sana wachezaji, mashabiki, mimi, na viongozi,"alisema.
Na mdadisiblog/festosaimon
Coutinho, Yondani wampasua kichwa Maximo

Sweetbert Lukonge na Goodluck Ngai
KOCHA Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo, amejikuta akitumbukia katika lindi la mawazo baada ya kuwakosa mazoezini nyota wake, Andrey Coutinho na Kelvin Yondani.
Wachezaji hao kwa pamoja jana walishindwa kufanya mazoezi na wenzao ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu Bara kutokana na kusumbuliwa na maradhi mbalimbali.
Hali hiyo imemfanya Maximo aonekane kuwa ni mwenye mawazo mengi kutokana na kutojua siku ambayo wachezaji hao ambao ni kati ya nyota wake wa kutumainiwa, watarudi uwanjani kuendelea na kazi yao.

Kelvin Yondani.
Daktari wa Yanga, Juma Sufiani, ameliambia Championi Jumamosi kuwa, wachezaji hao ni wagonjwa, ndiyo maana katika mazoezi ya jana hawakuweza kuonekana uwanjani.
Alisema Coutinho ambaye amejiunga na klabu hiyo hivi karibuni akitokea nchini Brazil, anasumbuliwa na maumivu ya mgongo wakati Yondani anasumbuliwa na Malaria.
“Hata hivyo, kwa sasa wanaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu, hivyo ni matumaini yetu kuwa watarudi uwanjani hivi karibuni kabla ya safari yetu ya kisiwani Pemba,” alisema Sufiani.
Kikosi hicho cha Yanga kinatarajia kuondoka Dar es Salaam manmo keshokutwa Jumatatu kwenda Pemba kwa ajili ya kupiga kambi ya siku 10 ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 20, mwaka huu.
Na mdadisiblog/festosaimon
Credit gpl
WASTARA AOLEWA NA MWANAUME ASIYEMJUA
Wastara alizaliwa mwaka 1983 katika Hospitali ya Turiani iliyopo wilayani Mvomero mkoani Morogoro akiwa ni mtoto wa tano kati ya saba waliozaliwa katika familia yao.
Staa katika tasnia ya filamu Bongo,Wastara Juma.
Alisoma Shule ya Msingi Mvomero na baada ya kuhitimu darasa la saba alijiunga na masomo ya sekondari katika Shule ya Sekondari Kibamba Agriculture ambapo alipofika kidato cha pili aliacha shule.
MATUKIO YA UTOTONI
Mwandishi: Unakumbuka utotoni mwako ni matukio gani ya hatari ambayo ulikuwa ukiyafanya?
“Nilikuwa naparamia miti ya miembe, mikorosho kama sina akili nzuri huko nilikuwa nafuata pia ngedere kwani nilikuwa nawapenda sana, nakumbuka nilishawahi kuvunjika miguu yote pia kuvunjika mkono wa kulia kwa kuparamia miti.”
SABABU ZA KUACHA SHULE
Mwandishi: Umesema uliacha shule ukiwa kidato cha pili, nini sababu?
“Niliacha shule baada ya rafiki yangu kuiba hela nyumbani kwao ambapo alikuwa anakuja nazo shuleni tunakula wote chips,
wazazi wake walipogundua wakaja kushtaki shuleni nikawa natafutwa ili nisimamishwe mbele ya wanafunzi wote nieleze na kuchapwa, nilipogundua hivyo sikwenda tena shuleni maana nilikuwa nina aibu sana.”
AUZA MADUKA
Mwandishi: Je, baada ya kuacha shule ulienda wapi?
“Mama yangu alikuwa mfanyabiashara, alikuwa na duka la nguo na lingine la kuuza madini hivyo nilienda kumsaidia kwenye maduka hayo.”
Mwandishi: Ulifanya hizo biashara kwa muda gani?
APATA MCHUMBA
“Nilifanya kwa muda wa miezi mitatu nikapatiwa mchumba nikaolewa japokuwa nilikuwa simpendi.’’
Mwandishi: Sasa ilikuwaje ukaolewa na mwanaume usiyempenda?
“Nakumbuka nilikuwa na miaka kumi na sita na sikuwahi hata kumuona wala kuzungumza na huyo mwanaume kabla ya ndoa,
alienda moja kwa moja kwa mama yangu wakakubaliana na wakati huo wazazi wakishaamua huwezi kupinga ,hivyo nililazimika kuolewa hivyohivyo kwani mama yangu alikuwa akiogopa aibu ya kuzalia nyumbani kwa vile kwa mila zetu sisi Waarabu ukiwa na miaka hiyo msichana unaonekana ni mkubwa na unastahili kuolewa.”(Wastara baba yake alikuwa Mwaarabu.)
MUME AMZIDI UMRI
Mwandishi: Huyo mwanaume wako mlikuwa mnalingana naye umri au alikuzidi?
“Mwanaume alikuwa mkubwa sana kwangu hivyo kutokana na udogo niliokuwa nao sikuwa najua nini maana ya ndoa kitu nilichokuwa najua kufanya ni usafi tu, suala la mapenzi ndiyo lilikuwa ni shughuli haswa kwani nilikuwa sijui.”
TENDO LA NDOA
Mwandishi: Sasa mumeo alipokuwa akitaka haki ya ndoa ulikuwa unafanyaje?
“Ilikuwa ni kama tunapigana wakati huo ukifika na nilipopata ujauzito sikutaka hata aniguse hivyo mpaka mtoto anazaliwa sikushiriki tena tendo la ndoa na huyo mwanaume kwani nilikuwa namwambia kwamba naumia.”
MAISHA MAGUMU
Mwandishi: Vipi sasa maisha ya ndoa yalikuwaje?
“Maisha yalikuwa magumu sana kwani mwanaume aliyenioa hakuwa na kazi ya aina yoyote na mama hakuligundua hilo, baada ya kunioa alikuwa anaenda kushinda nyumbani kwao ndiyo ndugu zake wakawa wanatupatia chakula na kutulipia kodi.
“Baada ya kuwa na ujauzito wazazi wake walinichukua, nikaenda kukaa nao Zanzibar lakini nikawa nateseka sana ambapo mama yangu aligundua na kusema nije Dar kwani anataka kuniona na kipindi hicho alikuwa anaumwa, nilikuja kwa mama aliponiona alihuzunika sana kwani nilikuwa nimedhoofika.

Teknolojia: Ifahamu Smartphone ya kwanza duniani ‘IBM Simon’ inayotimiza miaka 20 (picha)
mwanadamu kupitia simu hiyo ya kiganjani.Lakini yawezekana si wote ambao wanaifahamu
‘smartphone’ ya kwanza kuingia sokoni.

Smartphone ni nini?
Ni simu ya mkononi ambayo inauwezo wa kufanya mambo mengi yanayofanywa nakompyuta.
Smartphone ya kwanza
IBM Simon ndio ilikuwa ‘Smartphone’ ya kwanza duniani iliyoenda sokoni Agosti 16,
1994 na jan Agosti 16, 2014 ilitimiza miaka 20.

Hata hivyo IBM Simon ilikuwa haiitwi ‘Smartphone’ kipindi hicho, lakini ilikuwa na ‘features’ nyingi zilizoko kwenye ‘Smartphone’
za sasa.
“But it had a lot of the features we see today. It had a calendar, it could take notes and send emails and messages and combined all of this with a cell phone.” amesema Charlotte Connelly ambaye ni content developer wa makumbusho ya sayansi ya London.
IBM Simon ilikuwa na uzito wa gram 500. “It looks like a grey block but it’s not as big as
you’d imagine, It had a stylus and a green LCD screen, which is similar in size to the iPhone 4. In fact, it’s not a bad looking thing.”Aliongeza ms Connelly.

Charlotte Connelly, content developer wa makumbusho ya sayansi ya London.
Hata hivyo inasemekana ukubwa wa bei (kwa wakati huo) pamoja na maisha mafupi ya betri ni miongoni mwa sababu za kupotea haraka kwa simu hizo sokoni ndani ya miaka miwili baada ya kuzinduliwa.
IBM Simon ilikuwa ikiuzwa $899, na hapakuwa na internet ya simu wakati huo hivyo haikufanya vizuri. Ziliuzwa simu 50,000 tu na nyingi zilinunuliwa na wafanyabiashara.

Motorola ya 1984 (kushoto), IBM Simon ya 1994 (katikati) na simu za sasa 2014 (kulia)
Katika kuadhimisha miaka 20 ya IBM Simon,Makumbusho ya sayansi ya London, wataiweka
simu hiyo kama sehemu ya maonesho ya ‘Information Age’ mwezi Octoba mwaka huu.
IBM Simon ilitengenezwa na kampuni ya IBM pamoja na kampuni ya simu ya Marekani,
BellSouth. IBM wamesema waliita Simon kwasababu ilikuwa simple na iliweza kufanya karibu kitu
chochote mtu alichohitaji.
Na mdadisiblog/festosaimon
Alikiba: Nawaomba watu wasinikosanishe na Diamond, sina ugomvi naye!
tatizo na Diamond Platnumz na amewataka watu waache kuwakosanisha.

Akizungumza na mwandishi wetu jana, AliKiba amewataka watu kuachana na tabia ya
kuwagombanisha Diamond ili wafanye muziki mzuri.
“Kila mtu anaandika anachotaka juu ya mimi na Diamond, mpaka wengine wanatumia akaunti
fake za Facebook kutukosanisha, ndio maana nikasema kuna wengine wanafanya for fun na
wengine wanafanya ili kutukosanisha wengine
wanafanya lakini hawajui wanachofanya,”amesema Alikiba.
“Mimi najaribu kuwaomba wadau mbalimbali waache hiyo tabia ya kutukosanisha kwa sababu
mimi sina ugomvi na Diamond na wala sina mambo hayo.
Ninachowataka waendelee
kusupport kazi zetu ili mambo yaende vizuri kwa sababu sisi ndo wasanii wao tunaoiwakilisha Tanzania. Wanapotupa moyo
wao sisi tunazidi kukaza buti ili tufike mbali zaidi.
Watu wanaotengeneza ugomvi wangu na Diamond waache cha zaidi wafanye kusupport
muziki na watuambie ni mapungufu gani ambayo yamepungua ili tujirekebishe,”
ameongeza. Katika hatua nyingine, Alikiba amezungumzia
mapokezi ya wimbo Mwana na Kimasomaso pamoja na ujio wa video zake.
“Kwanza watu wamenipokea vizuri sana kama nilivyokuwa nikitarajia, imeonyesha ni jinsi gani yale malalamiko ya maana walikuwa
wakilalamika kwamba nimekumiss na nilivyotoa nyimbo watu wanasikiliza na kuinjoy na nyimbo
zenyewe zimekuja wakati mzuri na zenye maadili mazuri ya kuelimisha na kuchezeka na
ya kufurahisha.
Maandalizi ya video yapo tayari
na booking ipo tayari vilevile, maandalizi nimeandaa hata kabla sijatoa nyimbo, video itafanyika nje na moja ni hapa siwezi sema ni
nchi gani bado ni mapema nitasema baadae nikishaitoa, kwasababu nimetoa track mbili
moja itafanyika hapa na nyingine itafanyika nje.”
LIVERPOOL YASAJILI BONGE LA BEKI LA HISPANIA
BEKI wa pembeni wa Hispania, Alberto Moreno amesaini Liverpool kwa ada ya Pauni Milioni 12.
Makubaliano ya uhamisho huo yalifikiwa mapema wiki hii, lakini ikachukua muda hadi sasa klabu hiyo inamtambulisha rasmi mchezaji huyo.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 22 amekuwa akifanya vizuri kwa miaka miwili iliyopita - ikiwa ni pamoja na kuwamo kwenye kikosi cha U21 cha Hispania kiloichochukua ubingwa wa Ulaya mwaka 2013, na kung'ara Sevilla. Moreno alishinda taji la Europa League na Sevilla msimu uliopita na alimwaga machozi baada ya kufungwa na Real Madrid katika mechi ya UEFA Super Jumanne.
Na mdadisiblog/festosaimon
ASANTE KWA KUTEMBELEA BLOG HII ILI TUNAOMBA UJIUNGE NASI ILI KILA TUKIPATA HABARI ZIKUFIKIE KIRAHISI














