
Sweetbert Lukonge na Goodluck Ngai
KOCHA Mkuu wa Yanga, Marcio Maximo, amejikuta akitumbukia katika lindi la mawazo baada ya kuwakosa mazoezini nyota wake, Andrey Coutinho na Kelvin Yondani.
Wachezaji hao kwa pamoja jana walishindwa kufanya mazoezi na wenzao ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu Bara kutokana na kusumbuliwa na maradhi mbalimbali.
Hali hiyo imemfanya Maximo aonekane kuwa ni mwenye mawazo mengi kutokana na kutojua siku ambayo wachezaji hao ambao ni kati ya nyota wake wa kutumainiwa, watarudi uwanjani kuendelea na kazi yao.

Kelvin Yondani.
Daktari wa Yanga, Juma Sufiani, ameliambia Championi Jumamosi kuwa, wachezaji hao ni wagonjwa, ndiyo maana katika mazoezi ya jana hawakuweza kuonekana uwanjani.
Alisema Coutinho ambaye amejiunga na klabu hiyo hivi karibuni akitokea nchini Brazil, anasumbuliwa na maumivu ya mgongo wakati Yondani anasumbuliwa na Malaria.
“Hata hivyo, kwa sasa wanaendelea vizuri baada ya kupatiwa matibabu, hivyo ni matumaini yetu kuwa watarudi uwanjani hivi karibuni kabla ya safari yetu ya kisiwani Pemba,” alisema Sufiani.
Kikosi hicho cha Yanga kinatarajia kuondoka Dar es Salaam manmo keshokutwa Jumatatu kwenda Pemba kwa ajili ya kupiga kambi ya siku 10 ya kujiandaa na msimu ujao wa Ligi Kuu Bara unaotarajiwa kuanza kutimua vumbi Septemba 20, mwaka huu.
Na mdadisiblog/festosaimon
Credit gpl
0 comments:
Post a Comment