Alikiba anataka watu wafahamu kuwa hana na
tatizo na Diamond Platnumz na amewataka watu waache kuwakosanisha.

Akizungumza na mwandishi wetu jana, AliKiba amewataka watu kuachana na tabia ya
kuwagombanisha Diamond ili wafanye muziki mzuri.
“Kila mtu anaandika anachotaka juu ya mimi na Diamond, mpaka wengine wanatumia akaunti
fake za Facebook kutukosanisha, ndio maana nikasema kuna wengine wanafanya for fun na
wengine wanafanya ili kutukosanisha wengine
wanafanya lakini hawajui wanachofanya,”amesema Alikiba.
“Mimi najaribu kuwaomba wadau mbalimbali waache hiyo tabia ya kutukosanisha kwa sababu
mimi sina ugomvi na Diamond na wala sina mambo hayo.
Ninachowataka waendelee
kusupport kazi zetu ili mambo yaende vizuri kwa sababu sisi ndo wasanii wao tunaoiwakilisha Tanzania. Wanapotupa moyo
wao sisi tunazidi kukaza buti ili tufike mbali zaidi.
Watu wanaotengeneza ugomvi wangu na Diamond waache cha zaidi wafanye kusupport
muziki na watuambie ni mapungufu gani ambayo yamepungua ili tujirekebishe,”
ameongeza. Katika hatua nyingine, Alikiba amezungumzia
mapokezi ya wimbo Mwana na Kimasomaso pamoja na ujio wa video zake.
“Kwanza watu wamenipokea vizuri sana kama nilivyokuwa nikitarajia, imeonyesha ni jinsi gani yale malalamiko ya maana walikuwa
wakilalamika kwamba nimekumiss na nilivyotoa nyimbo watu wanasikiliza na kuinjoy na nyimbo
zenyewe zimekuja wakati mzuri na zenye maadili mazuri ya kuelimisha na kuchezeka na
ya kufurahisha.
Maandalizi ya video yapo tayari
na booking ipo tayari vilevile, maandalizi nimeandaa hata kabla sijatoa nyimbo, video itafanyika nje na moja ni hapa siwezi sema ni
nchi gani bado ni mapema nitasema baadae nikishaitoa, kwasababu nimetoa track mbili
moja itafanyika hapa na nyingine itafanyika nje.”
tatizo na Diamond Platnumz na amewataka watu waache kuwakosanisha.

Akizungumza na mwandishi wetu jana, AliKiba amewataka watu kuachana na tabia ya
kuwagombanisha Diamond ili wafanye muziki mzuri.
“Kila mtu anaandika anachotaka juu ya mimi na Diamond, mpaka wengine wanatumia akaunti
fake za Facebook kutukosanisha, ndio maana nikasema kuna wengine wanafanya for fun na
wengine wanafanya ili kutukosanisha wengine
wanafanya lakini hawajui wanachofanya,”amesema Alikiba.
“Mimi najaribu kuwaomba wadau mbalimbali waache hiyo tabia ya kutukosanisha kwa sababu
mimi sina ugomvi na Diamond na wala sina mambo hayo.
Ninachowataka waendelee
kusupport kazi zetu ili mambo yaende vizuri kwa sababu sisi ndo wasanii wao tunaoiwakilisha Tanzania. Wanapotupa moyo
wao sisi tunazidi kukaza buti ili tufike mbali zaidi.
Watu wanaotengeneza ugomvi wangu na Diamond waache cha zaidi wafanye kusupport
muziki na watuambie ni mapungufu gani ambayo yamepungua ili tujirekebishe,”
ameongeza. Katika hatua nyingine, Alikiba amezungumzia
mapokezi ya wimbo Mwana na Kimasomaso pamoja na ujio wa video zake.
“Kwanza watu wamenipokea vizuri sana kama nilivyokuwa nikitarajia, imeonyesha ni jinsi gani yale malalamiko ya maana walikuwa
wakilalamika kwamba nimekumiss na nilivyotoa nyimbo watu wanasikiliza na kuinjoy na nyimbo
zenyewe zimekuja wakati mzuri na zenye maadili mazuri ya kuelimisha na kuchezeka na
ya kufurahisha.
Maandalizi ya video yapo tayari
na booking ipo tayari vilevile, maandalizi nimeandaa hata kabla sijatoa nyimbo, video itafanyika nje na moja ni hapa siwezi sema ni
nchi gani bado ni mapema nitasema baadae nikishaitoa, kwasababu nimetoa track mbili
moja itafanyika hapa na nyingine itafanyika nje.”
0 comments:
Post a Comment