Simba SC wanajua sababu za msingi kwa nini walimtimua kocha Zdravko Logarusic kwa sababu ni wao wenyewe ndiyo walimuajiri, wao wanajua sababu za msingi kwa nini walikuwa na Loga, hilo ni juu yao kwa sisi ambao tupo nje ya klabu hatewezi kujua sababu hasa ya kufutwa kazi kwa Mcroatia huyo ambaye tayari alifanya kazi kwa kipindi cha nusu msimu wakati Simba ilipomaliza katika nafasi ya nne msimu wa 2013/14.
Kwa mtazamo wa haraka tu unaqwweza kupata sababu ambazo zimevunja mahusiano kati ya Simba na Loga.
Kwa nini Logarusic ametimuliwa Simba? Sababu zipo nyingi,
KIPIGO CHA MABAO 3-0 KUTOKA KWA ZESCO KATIKA ‘SIMBA DAY’
Haileti maana, na wala si kigezo cha kumuhukumu Logarusic kutokana na mchezo huo kwa sababu tangu mwaka 2009, Tamasha hilo lilipoanzishwa Simba imekuwa ni timu ya kufungwa tu. Haijawahi kushinda, vipi leo Logarusic aondolewe kwa sababu za matokeo mabaya katika mchezo huo dhidi ya Zesco ya Zambia. Simba kupteza mchezo huo haikuwa ‘ stori’.
MAHUSIANO MABAYA KATI YA LOGA NA WACHEZAJI
Kuna namna yake unaweza kulitazama suala hili, kiufundi na kiuweledi. Mahusiano kati ya kocha na wachezaji yanakujaje?. Nitatolea mfano nchi za wenzetu ambao soka linaendeshwa kitaalamu.
Mfano ni Luis Van Gaal, anatengeneza orodha ya wachezaji ambao anataka kuwa nao na kuipeleka kwa utawala, pia anaweka orodha ya wachezaji Fulani ambao wanakuwa huru kutafuta timu hata kama wana mikataba.
Marouane Fellaini, ni mfano mzuri katika hili kwa kuwa amepewa ruhusa ya kutafuta timu ambayo anaqweza kucheza. Van Gaaal anafanya hivyo kwa sababu baadhi ya wachezaji hao hawahitaji katika mfumo wake. Mfumo wake wa ufundishaji unawakataa wachezaji hao na hivyo inapelekea moja kwa moja wakose nafasi.
Turudi nyumbani, mfano ni Loga ni wachezaji wangapi ambao amegombana nao? Kwanini inakuwa hivyo? Kuna mazingira ambayo yanatengenezwa na viongozi wenyewe wa klabu ambao wamejiiingiza katika utamaduni husiokuwepo katika soka la kisasa kumsajilia mwalimu wachezaji Loga tayari amefanya kazi Simba kwa muda tangu alipochukua nafasi ya Abdallah King Kibadeni, mwishoni mwa mwaka uliopita.
Simba haikufanya vizuri chini yake, ilifanya vibaya. Moja ya matatizo ya Simba kufanya vibaya msimu uliopita ni kitendo cha uongozi uliokuwepo kufanya usajili na kufanya makocha kushindwa kuweka ,mbinu zao kwa sababu wachezaji wanaosajiliwa si wale ambao wanakuwa wakihitajika moja kwa moja.
Nafikiri, Simba walitakiwa kufikiria kabla ya kumpa mkataba wa mwaka mmoja zaidi. Kama walifikia uamuzi huo basi wangemuacha afanye usajili ili baadae mwalimu aweze kuwajibishwa kutokana na matokeo ya uwanjani Huwezi kunipa kazi bila vitendea kazi! Niwezeshe kila kitu kisha kaa pembeni nifanye kazi yangu. Lakini kwa Logan a Simba haikuwa hivyo.
Alikuwa akiletewa wachezaji na kuwakataa kutokana na kuwaona hawawezi kuendana na mbinu zake. Loga pia ana ‘ pointi’ ya msingi. NI wakati wa kujifunza kuhusu ‘ soka la kitaaalamu’.
UONGOZI MPYA
Nafikiri haukuwa na mipango na Logarusic japokuwa walimpatia mkataba wa mwaka mmoja, kufukuzwa kwake Juzi kumethibisha jambo hilo ambalo awali liliripotiwa katika mtandao huu.
Loga alipewa mkataba mpya baada ya kuwa nchini kwa wiki mbili, na habari za kutimuliwa kwake zilipoanza kuenea uongozi ukaamua kumpa mkataba ili kuzima uvumi hu. Lakin siku zote ‘ Muda unaongea’ na LOga ameingia katika ‘ taiming’ za wasio mtaka na kuwa muhanga wa kwanza wa mechi za ‘ Simba Day’.