Sunday, December 21, 2014

REAL MADRID MABINGWA WA DUNIA, WABEBA KOMBE AFRIKA

Unaweza kusema kweli huu ni mwaka wa Real Madrid, kwani wamefanikiwa kuitwanga San Lorenzo kwa mabao 2-0 na kubeba ubingwa wa dunia. Madrid wametupia mabao hayo mawili kupitia kwa Sergio Ramos na Gareth Balena kubeba Kombe hilo katika ardhi ya bara maarufu la Afrika. Mechi hiyo ya fainali ya Kombe la Dunia kwa klabu, imepigwa mjini Marakech, Morocco. Cristiano Ronaldo hakuweza kufunga katika mechi hiyo ambayo Madrid imeshinda mara 21 mfululizo. Kwa mwaka huu, Madrid imebeba makombe ya Ligi ya Mabingwa Ulaya, Copa del Rey na Super Cup ya Ulaya.

Posted via Blogaway

0 comments:

Post a Comment