Wednesday, November 12, 2014

Nuh mziwanda afunguka kuhusu kupewa kichapo na mpenzi wake kila anapokosea

MWANAMUZIKI wa Bongo Fleva, Nuh Mziwanda amefunguka kuwa watu wanaomsema vibaya kuhusu yeye kupewa kichapo na mpenzi wake, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ wanakosea kwani anaamini kufanywa hivyo ni mahaba. Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi karibuni, Mziwanda alisema kuna taarifa zimeenea kuwa huwa anapigwa na Shilole pindi anapokosea lakini ukweli si kupigwa ‘live’ bali ni kupigwa kimahaba. ‘Shilole’ akiwa na mpenzi wake ‘Nuh Mziwanda’. “Jamani kupigwa wanakozungumzia watu sielewi lakini mimi ananipiga kimahaba, wanaosema kuwa mpenzi wangu ananipiga washindwe, watuache kwa raha zetu,”alisema Shilole. Tupe maoni yako hapo Chini kuhusu wawili hawa..!!

0 comments:

Post a Comment