Wednesday, November 12, 2014
|
MWANAMUZIKI wa Bongo Fleva, Nuh Mziwanda
amefunguka kuwa watu wanaomsema vibaya
kuhusu yeye kupewa kichapo na mpenzi wake,
Zuwena Mohamed ‘Shilole’ wanakosea kwani
anaamini kufanywa hivyo ni mahaba.
Akizungumza na mwandishi wa habari hii hivi
karibuni, Mziwanda alisema kuna taarifa
zimeenea kuwa huwa anapigwa na Shilole pindi
anapokosea lakini ukweli si kupigwa ‘live’ bali ni
kupigwa kimahaba.
‘Shilole’ akiwa na mpenzi wake ‘Nuh Mziwanda’.
“Jamani kupigwa wanakozungumzia watu sielewi
lakini mimi ananipiga kimahaba, wanaosema
kuwa mpenzi wangu ananipiga washindwe,
watuache kwa raha zetu,”alisema Shilole.
Tupe maoni yako hapo Chini kuhusu wawili
hawa..!! |
0 comments:
Post a Comment