 |
| Vita ya maneno kati ya
Roy Keane na Alex Ferguson
sasa inazidi kuchanja
mbuga. |
 |
| Keane aliyekuwa nahodha wa
Manchester United
iliyopata mafanikio
makubwa chini ya Ferguson,
amesema kocha huyo ni
muongo.
Keane amesema hayo wakati
akizizundua kitabu chake
kipya cha Second Half.
Hajapoteza maneno au
kupepesa baada ya kusema
aliamua kitabu hicho baada
ya kusoma maneno mengi ya
uongo ya Ferguson kwenye
kitabu chake
kilichochapishwa mwaka
jana. |
 |
| “Ajabu kabisa, Ferguson
amepata mamilioni, amepata
jukwaa na sanamu kwenye
Uwanja wa Old Trafford,
hayo yote ni mafanikio.
“Sasa ni ajabu sana kama
anafikia hatua ya kuwasema
maneno mabaya watu
waliomsaidia kupata hayo
mafanikio.
“Kwangu nimeona si mambo
sahihi, hapaswi kufanya
hivyo na hakuwa sahihi.
“Hakika sikuwa nina mpango
wa kutoa kitabu, lakini
baada kitabu chake niliona
lazima nifanye hivyo,”
alisema Keane ambaye ni
kocha msaidizi wa Aston
Villa.
Katika kitabu hicho cha
Feguson (AMBACHO
HUTAFSIRIWA KWA KISWAHILI
NA GAZETI LA MICHEZO LA
CHAMPIONI), ameeleza namna
Keane alivyokuwa mkorofi
na asiyewakubali wachezaji
vijana. |
 |
| Ameeleza kuwa Keane
hakupenda wengine
wafanikiwe na alijisahau
baada ya yeye kumpa
uhuru. Pia alieleza na
kukiponda kitendo chake
cha kuwasakama wachezaji
wa Man United kwenye
mahojiano yake na runinga
ya klabu hiyo ya MUTV.
Lakini Keane amesema yote
hayo ni uzushi mtupu na
ameyajibu kwenye kitabu
chake hicho cha Second
Half. |
KAMA BADO UJAJIUNGA NASI ILI KILA TUKIPATA HABARI ZIKUFIKIE KIRAHISI KWENYE FACEBOOK YAKO BOFYA HAPA
0 comments:
Post a Comment