Wednesday, October 15, 2014

Mama Kanumba na Lulu katika filamu mpya "Mapenzi ya Mungu"

Hivi karibu msanii mahiri na nguli katika tasnia ya filamu nchini Elizabeth Michael almaarufu kama Lulu ataibuka na filamu yake Mpya na yenye kusisimua iitwayo "MAPENZI YA MUNGU" ambapo moja kati ya washiriki katika filamu hiyo ni Bi Flora Mtegoha ambaye ni Mama Mzazi wa aliyekuwa msanii nguli wa kiume hapa 'Bongo' marehemu Steven Kanumba. Filamu ya "Mapenzi ya Mungu" ni moja ya filamu ambayo Lulu ameonesha uwezo wa hali ya juu na kuthibitisha kuwa ni mmoja kati ya wasanii wa kike hapa Tanzania ambaye ana kipaji cha hali ya juu katika kuuvaa uhusika ambapo ana uwezo wa kubadilika badilika kutokana na muongozo anaopewa. Filamu ya "Mapenzi ya Mungu" itakuwa sokoni hivi karibuni kwa wauzaji wa filamu kote nchini. Filamu hii itasambazwa na Kampuni mahiri ya Proin Promotions Ltd.

0 comments:

Post a Comment