Tuesday, September 16, 2014
|
Mwili wa Melasi Lutebula Ndabi ukiwa
umetupwa baada ya kuchinjwa.
Mfanyabiashara aliyefahamika kwa jina
la Melasi Lutebula Ndabi ambaye pia
alikuwa Mwenyekiti wa Kamati ya
Ulinzi na Usalama Mtaa wa Muhimbili 2,
Kata ya Pemba, Wilaya ya Temeke jijini
Dar, ameuawa kwa kuchinjwa na watu
wanaodaiwa kufika kwake kwa ajili ya
kukodi shamba la kulima matikiti.Habari
zinadai kuwa, marehemu mbali na kuwa
mfanyabishara na kiongozi katika eneo
hilo, pia alikuwa akijishughulisha kwa
kilimo na ufugaji, kazi ambazo amekuwa
akizifanya tangu afike katika eneo hilo
mwaka 2005.
Akizungumza kwa uchungu na Uwazi,
mke wa marehemu aitwaye Rehema
Shaban (pichani), alisema siku za nyuma
kuna watu watatu walifika nyumbani
hapo wakihitaji kukodi shamba kwa ajili
ya kulima matikiti.
Watu hao ambao inadaiwa si wakazi wa
eneo hilo na wala hawajulikani walisema
wanatokea Kijiji cha Lisu wilayani
Nzega, Mkoa wa Tabora walielekezwa
kwa marehemu huyo.
Ilielezwa kuwa, kwa mara ya kwanza
watu hao walifika nyumbani kwa
marehemu Septemba 5,
mwaka huu baada ya mazungumzo ya
kina, marehemu aliwaonesha eneo la
ekari tatu. |
Posted via Blogaway
0 comments:
Post a Comment