Tuesday, September 02, 2014
|
Siku ya mwisho ya usajili barani ulaya
imefungwa kwa staili ya aina yake na klabu ya
Manchester United baada ya kufanikiwa
kumsajili mshambuliaji wa kimataifa wa
Colombia Radamel Falcao.
United ambao leo hii imewauza washambuliaji
wake wawili Chicharito na Danny Welbeck –
imethibitisha kumsajili Falcao kwa mkataba wa
mwaka mmoja kwa mkopo huku wakiwa na
option ya kumnunua moja kwa moja msimu
ujao.
Falcao anakuwa mchezaji wa sita kujiunga na
Man United wakati wa dirisha hili la usajili,
baada ya Luke Shaw, Herrera, Blind, Di Maria,
na Rojo.
Kocha Louis Van Gaal amesema mchezaji wa
aina ya Falcao anakupokuwa na uwezekano wa
kumpata basi hiyo sio nafasi ya kuipoteza.
Falcao nae alisema: “Nina furaha kujiunga na
Manchester United kwa mkopo. Manchester
United ni klabu kubwa zaidi duniani na ina
kila sababu ya kurudi kuwa juu tena. Nipo
tayari kufanya kazi na Louis van Gaal na
kuisadia timu kupata mafanikio katika kipindi
nitakachokuwepo kwenye klabu.” |
BONYA HAPA KUHUNGANA NASI ILI UPATE HABARI KIRAHISI PUNDE ZITUFIKIAPO
0 comments:
Post a Comment