Tuesday, September 02, 2014
|
Dirisha la usajili barani ulaya limefungwa
usiku wa jana – Shinji Kagawa ni mmoja wa
wachezaji waliofanya uhamisho katika dirisha
hili la usajili.
Kiungo wa Japan, aliuzwa kutoka Manchester
United kwenda Borussia Dortmund kwa ada ya
uhamisho wa £6.3million.
Fedha hizo walizolipa Dortmund zinaweza
kuwa zimerudi ndani ya siku kadhaa baada ya
ripoti ya gazeti la BILD kusema kwamba
mauzo ya jezi namba 7 atakayoivaa Kagawa
akiwa Dortmund yamekuwa ya kasi mno.
Ripoti zinasema jezi ya Shinji Kagawa iliuzwa
mpaka kufikia idadi ya jezi 5,000 katika
kipindi cha masaa kadhaa tangu alipotangazwa
rasmi kurudi kwenye klabu yake hiyo
aliyohama na kwenda United mnamo mwaka
2010. |
0 comments:
Post a Comment