Tuesday, September 16, 2014
|
Na Boniface Wambura, DAR ES SALAAM
KAMATI ya Sheria na Hadhi za Wachezaji ya
Shirikishola Soka Tanzania (TFF), imewapa
siku 14 Simba SC kumaliza mgogoro wao na
kocha wao wa zamani, Mcroatia Zdravko
Logarusic.
Taarifa ya TFF leo, imesema kwamba iwapo
pande hizo mbili zitashindwa kufikia
mwafaka ndani ya siku 14, suala hilo
litarejea tena mbele ya Kamati.
Logarusic aliyewakilishwa na mwanasheria
wake Dickson Sanga anailalamikia klabu
hiyo kwa kuvunja mkataba kinyume cha
taratibu, hivyo kutaka Simba imlipe dola
6,000 kwa kuvunja mkataba, na pia kulipa
dola 50,000 ikiwa ni fidia maalumu ya
madhara yaliyotokana na uvunjwaji huo.
Simba SC ilimfukuza Logarusic mwezi
uliopita baada ya kufanya kazi tangu
Desemba mwaka jana, ikidai kwamba
haendani na maadili ya klabu hiyo.
Aidha, Kamati pia imepitisha usajili wa
wachezaji wa klabu za Ligi Kuu na Ligi
Daraja la Kwanza huku wenye kasoro
ndogondogo klabu zao zikitakiwa kuziondoa
ili waweze kupatia leseni za kucheza ligi
msimu huu wa 2014/2015.
Kasoro hizo ni kufikia makubaliano na
klabu ambazo wachezaji husika wametoka,
kuwafanyia uhamisho (transfer) na kulipa
ada za uhamisho. Kamati vilevile ilibaini
wachezaji wengi hawakufanyiwa uhamisho
kama kanuni za ligi hizo zinavyoelekeza.
Hivyo, klabu ambazo hazitakuwa zimeondoa
kasoro hizo kwa wachezaji wao leseni zao
zitazuiliwa mpaka watakapokuwa
wamekamilisha kila kitu. Ni wachezaji
wenye leseni tu ndiyo watakaoruhusiwa
kucheza mechi za ligi.
Klabu za African Lyon, African Sports,
Ashanti United, Coastal Union, Kiluvya
United, Majimaji, Mji Mkuu, Polisi Dodoma,
Polisi Morogoro, Red Coast na Stand United
ziliwawekea pingamizi wachezaji mbalimbali
kwa kutofanyiwa uhamisho.
Kuhusu Ike Bright Obina wa Nigeria
aliyewekewa pingamizi na African Lyon
dhidi ya Coastal Union, Kamati imezitaka
klabu hizo kufikia makubaliano, na
zikishindwa mchezaji huyo atabaki African
Lyon. |
Posted via Blogaway
0 comments:
Post a Comment