Monday, September 01, 2014

KIFAA KINGINE CHA CHELSEA CHAENDA AC MILAN KWA MKOPO

KINDA wa Chelsea, Marco van Ginkel amekamilisha uhamisho wa mkopo kwenda AC Milan, akifuata nyayo za Fernando Torres. Kiungo huyo wa Uholanzi, Van Ginkel sehemu kubwa ya msimu wake wa kwanza Stamford Bridge alikuwa anasumbuliwa na majeruhi na hivyo kocha Jose Mourinho ameamua kumtoa akapate uzoefu. Kuondoka kwa mchezaji huyo kunapunguza idadi ya wachezaji wa kigeni ili waweze kuendana na kanuni za mashindano ya Ligi Kuu ya England na Ligi ya Mabingwa Ulaya.

0 comments:

Post a Comment