Friday, September 05, 2014

HIKI NDO KITU KINACHO ENDELEA MAN UNITED KUHUSU MARCOS ROJO

BEKI mpya wa Manchester United, Marcos Rojo anaweza kuichezea kwa mara ya kwanza klabu yake hiyo katika mchezo wa Ligi Kuu ya England dhidi ya Queens Park Rangers Uwanja wa Old Trafford Septemba 14 baada ya kupatiwa hati ya kufanya kazi. Rojo alisafiri hadi Lisbon Alhamisi ili kukamilisha taratibu za kupata hati hiyo ya kufanyia kazi England. Kufanikiwa kwa mchezaji huyo kupata hati hiyo ya kufanyia kazi ni faraja kwa kocha Louis van Gaal, ambaye kikosi chake mina tatizo la safu ya ulinzi.

Posted via Blogaway

0 comments:

Post a Comment