Thursday, September 04, 2014

HAYA NDO MAPYA ALIYOYAZUA OKWI LEO HII JAGWANI

YANGA imesikia maneno ya straika wake wa zamani, Emmanuel Okwi, aliyejiunga na Simba na imemuahidi hatocheza mechi za Ligi Kuu Bara labda mazoezi na mechi za kirafiki tu za timu aliyojipeleka. Mapema Okwi aliliambia gazeti hili kwamba ana uhakika ataichezea Simba msimu ujao wa ligi kuu utakaoanza Septemba 20 na akawaambia mashabiki wa Yanga atawafanya kitu kibaya katika mechi dhidi yao Oktoba 12 pale Uwanja wa Taifa. Lakini wakati Okwi akiamini hivyo, Yanga imemjibu kuwa asijidanganye hata kidogo kwani ataishia kucheza mazoezi na mechi za kirafiki tu kwa kuwa wana uhakika juu ya maeneo yatakayowapa ushindi katika mgogoro wao. Mmoja wa mabosi wa juu wa Yanga anayefanya kazi kwa karibu na Mwenyekiti wa timu hiyo, Yusuf Manji ameliambia Mwanaspoti kuwa hawajashtuka hata kidogo juu ya kauli ya Okwi kwani ana uhakika wa kisheria kuwa mchezaji huyo ataitumikia Simba katika mechi za kirafiki tu. Atakavyonaswa Okwi Bosi huyo alisema hawataki kulumbana na Okwi wala Simba, lakini uongozi wao umejikamilisha vya kutosha kuweza kuishinda vita hiyo ambapo kwanza watatumia mawasiliano ya Okwi alipozungumza na klabu ya Wadigalde FC ya Misri ambayo mchezaji huyo alitaja kiasi cha fedha Dola 60,000 ambazo Yanga ingepatiwa endapo ingekubali kumuuza. “Tumemsikia anachoongea tusubiri tuone kama atacheza huko Simba, unajua Yanga tunafanya kazi kwa mfumo bora, Okwi anatakiwa kutambua kuwa tunayo barua pepe yake ambayo alituarifu juu ya kutakiwa na hiyo timu ya Misri tena akaenda mbali zaidi kwa kutaja mpaka kiasi cha fedha kitakachotolewa na hiyo timu anawezaje kukataa kwamba hakuzungumza nao?” Alihoji. “Pili akumbuke mkataba una kipengele kinachosema mchezaji husika mkataba wake utaanza kutumika pale tu atakapoanza kuitumikia timu na kuhusu vibali vya kuchezea hilo ni jukumu lake kuvifuatilia akivikosa ataturudishia fedha zetu, alipokuja hapa akazuiwa kucheza ni kosa letu au lake?” Aliongeza eneo la tatu ambalo Yanga litawapa ushindi ni kuwa Okwi hana nakala ya barua ikionyesha klabu yao kutaka kuvunja mkataba. “Nimemsikia siku aliyokuwa akitambulishwa akidai tulivunja mkataba wake, anatakiwa kutambua mkataba wake na klabu yetu hatuwezi kuuvunja TFF bila ya kukutana naye, wapi atatuonyesha kwamba tulimwandikia tukitaka kuvunja mkataba wetu?” alihoji. Phiri amtumia Okwi Kocha wa Simba, Patrick Phiri amesema Okwi ni mchezaji mahiri na tayari amemuweka katika programu zake.

Posted via Blogaway

0 comments:

Post a Comment