 |
WINGA Angel di Maria ametengeneza mabao
matatu na kufunga moja, Argentina ikilipa
kisasi cha Kombe la Dunia kwa kuifunga 4-2
Ujerumani usiku huu katika mchezo wa kirafiki
mjini Dusseldorf, Ujerumani.
Mchezaji huyo ghali zaidi kuwahi kusajiliwa
Manchester United na Uingereza nzima alipika
mabao ya Sergio Aguero, Erik Lamela na
Federico Fernandez kabla ya kufunga na lake
mwenyewe siku 52 tangu bao la Mario Gotze
katika muda wa nyongeza liipe Ujerumani
ubingwa wa dunia nchini Brazil.
Mabao matano kati ya sita yamefungwa na
wachezaji wa Ligi Kuu ya England, huku Andre
Schurrle akiifungia Ujerumani kabla ya Gotze
kuwafungia bao la pili mabingwa hao wa
dunia. |
KAMA BADO UJAJIUNGA NASI BOFYA HAPA ILI KILA NIKIPATA HABARI ZIKUFIKIE KIRAHISI PUNDE NIZIPATAPO
Posted via Blogaway
Sheeedah
ReplyDelete